Thursday, January 2, 2014

CCM Rorya yawatahadharisha wale wanaoleta Makundi ndani ya Chama


RORYA

                              Bw Samweli Kiboye - Mwenyekiti wa Chama

Chama cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Rorya Mkoani Mara kimewataka wanachama na wapenzi wa Chama hicho kuungana katika Mwaka 2014 kuhakikisha Chama hicho kinafanya vizuri katika Chaguzi zinazokuja huku kikiwatahadharisha wale wote wenye kuleta Makundi ndani ya Chama.

Kauli hiyo ilisemwa na Mwenyekiti wa Chama Mapinduzi CCM wilaya Rorya Bw Samweli Kiboye katika kikao cha halmashauri kuu cha wilaya hiyo kilichofanyika Mwishoni mwa Mwaka 2013 katika wilaya hiyo.

Amesema kama Chama hicho kitawaogopa wale wote wanaleta Makambi ndani ya Chama kazi itakuwa ngumu kwa Chama hicho katika chaguzi zinazokuja 

"Kumekuwa na watu wasiotakia CCM mema wamekuwa wakileta makundi makundi tu ndani ya Chama,sasa hatutakubali wale wote wanaoleta Makundi ndani ya Chama"alisema Mwenyekiti huyo
                                Baadhi ya wanaCCM wakiwa katika halmashauri kuu

Kwa Upande wake Katibu wa CCM katika wilaya hiyo Dr Fikirini Masokola alisema kiongozi yeyote wa Serikali ambaye atashindwa kutimiza Matarajio ya Chama hicho ndani ya wilaya ya Rorya hawatahitaji kuwa nae katika wilaya hiyo.

 "Hatutakubali kuwa  na kiongozi yoyote ambaye hatatimiza Matakwa ya Serikali kwa wanaRorya" alisema Dr Fikirini Masokola

Katika Kikao hicho Chama cha Mapinduzi CCM kilitoa hati ya Pongezi kwa  baadhi ya watu ambao wametoa ushirikiano ndani ya Chama hicho kwa Mwaka 2013 huku kikiwaomba kuendeleza ushirikiano wao katika Chama hicho kwa Mwaka 2014

No comments:

Post a Comment