Thursday, September 26, 2013

AJALA MBAYA ILIVYOTOKEA LEO ASUBUHI BARABARA YA MAJITA KARIBU NA MAKAZI YA MKUU WA MKOA,KUMRADHI KWA PICHA








                                   ASKARI WA USALAMA BARABARANI WAKITOA MSAADA






Ajali mbaya imetokea asubuhi ya leo majira ya saa 2 kwenye barabara ya majita karibu na makazi ya mkuu wa mkoa wa Mara baada ya gari aina ya VX land cruser namba T 901 AHH kuigonga pikipiki iliyokuwa ikitoka maeneo ya mjini musoma kuelekea kamnyonge.
Kamera yetu imemshuhudia majeruhi wa ajali aliyedaiwa kuwa ni abiria akiwa anavuja damu nyingi kichwani huku akipumua kwa shida na muda mchache askari wa kikosi cha usalama barabarani walifika eneo la tukio na kumchukua kwa ajili ya kumuwahisha hospitali.
Mashuhuda walioshuhudia ajali hiyo kabla ya camera ya bloog hii kufika eneo la tukio muda mchache wamesema dereva wa pikipiki ambaye alidaiwa kupakia abilia alitaka kulipita gari hilo na kuingia eneo la gari hali iliyopelekea kutokea kwa ajali hiyo.
Mmoja wa mashuhuda wa ajali hiyo dereva wa pikipiki Wambura Matiku aliyekuwa nyuma ya pikipiki iliyopata ajali aliiambia blog hii dereva wa pikipiki mara  baada ya kulipita gari hilo aliwahi kuingia upande wa gari na kutokea kwa ajali hiyo.
Hata hivyo jeshi la polisi mara baada ya kumuwahisha majeruhi huyo hospitalini walirejea eneo la tukio na kupima ili kubaini chanjo cha ajali hiyo huku Kamanda wa polisi Mkoa wa Mara Ferdinand Mtui akiahidi kuhitolea taarifa mara baada ya kubaini chanzo cha ajali hiyo

No comments:

Post a Comment