Sunday, July 14, 2013

MACHIMBO YA KOKOTO YAUA WAWILI,MMOJA MAJERUHI WOTE WA FAMILIA MOJA.

JOSEPH WAMBURA NDUGU WA MAREHEMU NA MAJERUHI AKIWA AMELAZWA WODI LA WANAUME BAADA YA KUPOTEZA FAHAMU MUDA MFUPI TU BAADA YA KUFIKA ENEO LA TUKIO NA KUSHUHUDIA VIFO.

Julai 14,2013.
Serengeti:WATU wawili wakazi wa kitongoji cha Kanisani kijiji cha Matare Mamlaka ya mji wa Mugumu wilayani Serengeti wa familia moja  wamekufa na mmoja kujeruhiwa baada ya kuangukiwa na kifusi wakati wakichimba kokoto.
Tukio hilo limethibitishwa na polisi,uongozi wa kitongoji na Hospitali teule ya Nyerere ddh limetokea julai 14 majira ya saa 4:10 asubuhi mwaka huu katika eneo la machimbo ya kokoto,wakati wakiwa wanachimba.
Mwenyekiti wa kitongoji hicho Juma Mahando amewataja waliofariki kuwa ni Rhobi Mwita Nyantori(45)ambaye alifia eneo la tukio,Nyahiri Chacha Mwita(41)ambaye amefariki baada ya kupata huduma na majeruhi ni Wegesa Mwita(39)ambaye amelazwa.
Akisimulia mkasa huo kwa kugugumia Wegesa ambaye ni majeruhi alisema wenzake walikuwa ndani ya shimo nay eye akiwa pembeni akisubiri mzigo wa kokoto aweze kutoa nje ghafla walianguliwa na kifusi chote na kuwafunika.
“Udongo wote umenifunika..kilichosaidia pembeni kulibaki kama uwazi,lakini waliokuwa ndani humo umewapiga wakiwa wameinama na kuanguka…watu waliokuwa nje waliona na kupiga kelele wakajitokeza watu wakatupa msaada…nahisi maumivu makali kiunoni na mbavu”alisema kwa kugugumia.
Mganga wa zamu dk,Amosi Kittoh amesema kilichopelekea kifo cha Rhobi ni kuumia kifuani na Nyahiri alipata madhara makubwa kwenye uti wa mgongo .
Dk ,Kittoh amesema kuwa tukio hilo limesababisha ndugu wa marehemu hao Joseph Wambura kupoteza fahamu na wamemlaza wodi ya wanaume kwa ajili ya matibabu.
Akizungumzia machimbo hayo Mwenyekiti wa kitongoji hicho Mahando alisema novemba 2009 watu wawili wa familia moja waliangukiwa na kufariki,ikiwa ni mwendelezo wa matukio ya vifo na serikali ikayafunga.
Hata hivyo alisema watu walikuwa wakienda kuchimba kama wizi kujipatia riziki,hata hivyo baadhi ya wananchi walisema serikali inafahamu kuwa machimbo hayo yanaendelea kwa kuwa kokoto huuzwa hadharani,huku hata viongozi wa wilaya wakiwa ni wateja wao na ndiyo maana yameendelea kwa kipindi chote bila kuwakamata wahusika.
Mwisho.
Wegesa Mwita(39)mmoja wa majeruhi ambaye amelazwa,katika hospitali teule ya Nyerere ddh baada ya kuangukiwa na kifusi wakichimba kokoto,akisukumwa na mwenyekiti wa kitongoji cha kaniasani Matare wilayani Serengeti Juma Mahando.


 Wegesa Mwita(39)majeruhi katika tukio hilo.
 BAADHI YA NDUGU WAKILIA BAADA YA KUTAARIFIWA KUFARIKI KWA NYAHIRI CHACHA MWITA(41)

source Mayunga Blog

No comments:

Post a Comment