Tuesday, June 4, 2013

NEYMAR ATAKA KUMFANYA MESSI AENDELEE KUWA MCHEZAJI BORA WA DUNIA, ATAMBULISHWA RASMI KWA MKATABA WA MIAKA MITANO!!


Nyota wa Brazil Neymar Da Silva ametambulishwa leo katika klabu ya Barcelona na kuungana na nyota wa miamba hiyo ya Dunia Andrew Lionel JorgE Messi ambapo watacheza katika safu hatari ya ushambuliaji.

Nyota huyo mwenye kipaji cha hali ya juu amesaini mkataba wa miaka mitano kuitumiki klabu yake mpya baada ya kufanya kazi iliyotukuka katika timu ya Santos ya kwao Brazil.

Neymar alisafiri jana usiku baada ya kumalizika kwa mechi ya kirafiki ya timu yake ya taifa ya Brazil dhidi ya England iliyomalizika kwa sare ya kufungana mabao 2-2 na leo hii imefuzu vipimo katika klabu ya Barca na kutambulishwa mbele ya umati mkubwa wa mashabiki wa klabu hiyo katika dimba la Camp Nou.

Katika mahojiano na waandishi wa habari baada ya kutambuliwshwa rasmi, Neymar alisema “Nimekuja hapa kumsaidia na kumsaidia Messi ili aendelee kuwa mchezaji bora wa dunia”.
Neymar alisisitiza kuwa amefurahi sana kuwa mchezaji wa Barcelona kwani ilikuwa ndoto yake, hivyo ataifanyia makubwa zaidi na kuifanya endelee kuwa klabu bora zaidi duniani.

Kazi imebaki kwa kocha Tito Vilanova kufanya maamuzi jinsi atakavyowachezesha nyota hao wawili, lakini kiungo fundi Andres Iniesta ana uwezo wa kuwalisha wote wawili mipira ya maana endapo watacheza pamoja.
Arrival: Neymar was unveiled as a Barcelona player at the Nou Camp on MondayAmefika kwa mafundi wenzake: Neymar ametambulishwa rasmi leo Camp Nou na kujiunga na nyota wa dunia Lionel Messi
Welcome: The Brazilian has signed a five-year deal with the Catalan clubKaribu Camp Nou: Mbrazil Neymar amesaini mkataba wa miaka mitano kuichezea Barca ya Messi
Juggling: Neymar showed off his skills to the Nou Camp crowdMaufundi ya kufa mtu: Neymar alionesha kipaji cha hali ya juu leo Camp Nou, alichezea gozi kama kazaliwa nalo

FC Barcelona's new signing Neymar
Nyota huyo amefuzu vipimo vya afya na anatarajiwa kuanza kuitumika klabu ya Kalalunya juni 28 mwaka huu, na leo hii amepimwa mbele ya rais wa Barca, Sandro Rosell, Makamu wake, Josep Maria Bartomeu na mkurugenzi wa michezo, Andoni Zubizarreta.
Mpaka sasa ada ya uhamisho haijawekwa wazi

Dynamic duo: Neymar will join Lionel Messi in a formidable partnership for BarcelonaDaaah! nyota huyu na mwenzake: Neymar anajiunga na Lionel Messi kuongoza safu hatari ya ushambukiaji ya Baraca
Meet and greet: Barcelona's president Sandro Rosell welcomes Neymar to the Nou CampFulu shangwe: Rais wa Barcelona, Sandro Rosell amemkaribisha Neymar, Nou Camp
Crowd: Neymar waves to the fans gathered at the Nou Camp as he walks onto the pitch for the first timeNyomi kubwa mnooo!: Neymar akiwapungia mkono mashabiki wa Barcelona waliofurika Camp Nou na kwa mara ya kwanza ametembea katika dimba hilo


Fans: Neymar highfives young supporters on the Nou Camp pitchMadogo wanaoshabikiwa Barca: Neymar akiwa hai mashabiki watoto wa Barca katika dimba la Camp Nou
Put through his paces: Neymar passed his medical before being unveiled on the pitchVipimo vya afya: Neymar amefuzu zoezi hilo.

Put through his paces: Neymar passed his medical before being unveiled on the pitch

Fuulshangwe

No comments:

Post a Comment