Nyota
wa Brazil Neymar Da Silva ametambulishwa leo katika klabu ya Barcelona
na kuungana na nyota wa miamba hiyo ya Dunia Andrew Lionel JorgE Messi
ambapo watacheza katika safu hatari ya ushambuliaji.
Nyota
huyo mwenye kipaji cha hali ya juu amesaini mkataba wa miaka mitano
kuitumiki klabu yake mpya baada ya kufanya kazi iliyotukuka katika timu
ya Santos ya kwao Brazil.
Neymar
alisafiri jana usiku baada ya kumalizika kwa mechi ya kirafiki ya timu
yake ya taifa ya Brazil dhidi ya England iliyomalizika kwa sare ya
kufungana mabao 2-2 na leo hii imefuzu vipimo katika klabu ya Barca na
kutambulishwa mbele ya umati mkubwa wa mashabiki wa klabu hiyo katika
dimba la Camp Nou.
Katika
mahojiano na waandishi wa habari baada ya kutambuliwshwa rasmi, Neymar
alisema “Nimekuja hapa kumsaidia na kumsaidia Messi ili aendelee kuwa
mchezaji bora wa dunia”.
Neymar
alisisitiza kuwa amefurahi sana kuwa mchezaji wa Barcelona kwani
ilikuwa ndoto yake, hivyo ataifanyia makubwa zaidi na kuifanya endelee
kuwa klabu bora zaidi duniani.
Kazi
imebaki kwa kocha Tito Vilanova kufanya maamuzi jinsi atakavyowachezesha
nyota hao wawili, lakini kiungo fundi Andres Iniesta ana uwezo wa
kuwalisha wote wawili mipira ya maana endapo watacheza pamoja.
![Arrival: Neymar was unveiled as a Barcelona player at the Nou Camp on Monday](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/06/03/article-2335272-1A2122C2000005DC-690_634x464.jpg)
![Welcome: The Brazilian has signed a five-year deal with the Catalan club](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/06/03/article-2335272-1A211E71000005DC-284_634x437.jpg)
![Juggling: Neymar showed off his skills to the Nou Camp crowd](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/06/03/article-2335272-1A2135E9000005DC-254_634x447.jpg)
![FC Barcelona's new signing Neymar](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/06/03/article-2335272-1A213502000005DC-728_634x409.jpg)
Mpaka sasa ada ya uhamisho haijawekwa wazi
![Dynamic duo: Neymar will join Lionel Messi in a formidable partnership for Barcelona](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/06/03/article-2335272-15663948000005DC-549_634x491.jpg)
![Meet and greet: Barcelona's president Sandro Rosell welcomes Neymar to the Nou Camp](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/06/03/article-2335272-1A2118E9000005DC-602_634x329.jpg)
![Crowd: Neymar waves to the fans gathered at the Nou Camp as he walks onto the pitch for the first time](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/06/03/article-2335272-1A212676000005DC-328_634x411.jpg)
![Fans: Neymar highfives young supporters on the Nou Camp pitch](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/06/03/article-2335272-1A21285D000005DC-431_634x471.jpg)
![Put through his paces: Neymar passed his medical before being unveiled on the pitch](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/06/03/article-2335272-1A20F000000005DC-938_634x458.jpg)
![Put through his paces: Neymar passed his medical before being unveiled on the pitch](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/06/03/article-2335272-1A20EF87000005DC-580_634x439.jpg)
Fuulshangwe
No comments:
Post a Comment