Watu wawili
wamekufa katika Matukio tofauti Manispaa ya Musoma Mkoani Mara,taarifa ya Jeshi
la Polisi mkoani hapa kwa Waandishi wa habari imeeleza kuwa tukio la Kwanza Mtu
mmoja mwendesha Pikipiki ameokotwa akiwa amekufa katika eneo la Rwamlimi
Manispaa ya Musoma mkoani hapa.
Taarifa ya
tukio hilo inaeleza kuwa Marehemu aliyekuwa anafahamika kwa jina la Maendeleo
Yohana umri miaka 45 aliokotwa huku Miguu na Mikono yake ikiwa imefungwa
Kamba.Mnamo April 27 majira ya saa mbili usiku Marehemu aliitwa na Mteja kwenda mahali alikofia.
Katika
taarifa hiyo imeeleza kuwa mpaka sasa jeshi hilo linamshikilia mtu mmoja
kutokana na tukio hilo,wakati huo huo taarifa hiyo imeeleza kuwa Mama mmoja
aliyefahamika kwa jina la Regina Manyama miaka 67 amechinjwa hadi kutengenisha
shingo na Kiwiliwili na watu wasiojulikana.
Katika tukio
la tatu taarifa hiyo inaeleza kuwa Binti mmoja anayekadiriwa kuwa na umri wa
miaka 20 na asiyefahamika kwa majina,kabila wala Makazi amekutwa amekufa katika
eneo la Mgaranjabo Manispaa ya Musoma mkoani Mara na maiti yake kuharibika huku
Maiti yake ikiwa pembeni ya mfereji wa maji jirani na eneo la kuchimbia
mchanga.
Mwili wa
marehemu huyo umekutwa ukiwa uchi na chanzo cha kifo kinachunguzwa ambapo mpaka
sasa hakuna anayeshikiliwa na jeshi hilo.
Kufuatia
Matukio hayo ya Mauaji,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mara ameoa wito kwa wananchi
huku akihimiza wenye taarifa za siri kuzitoa ili wahusika wafikishwe kwenye
vyombo vya sheria
No comments:
Post a Comment