Sunday, April 14, 2013

KAULI YA FERGUSON KUHUSU USAJILI WA FALCAO

.
.
Kocha wa Manchester United Sir Alex Fergusson amekanusha taarifa zilizosambaa kwenye vyombo Vya habari barani ulaya za klabu yake kuwa mbioni kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa Colombia na klabu ya Atletico Madrid Radamel Falcao.

Fergusson amekanusha taarifa hizo kwenye mkutano na waandishi wa habari ambapo alisema kuwa yeye mwenyewe ameshangazwa na taarifa hizo ambazo amethibitisha kuwa hazina ukweli wowote kwani hadhani kama United ina nafasi ya mshambuliaji mwingine .
Wiki iliyopita gazeti la michezo la Hispania Marca liliandika taarifa kuwa Manchester United inafanya mpango wa kumsajili Falcao ambapo ilikuwa tayari kulipa paundi milioni 27 pamoja na mshambuliaji wa Mexico Javier Hernandez Chicharito .

Gazeti hilo (Marca) lilisema kuwa United tayari imeanza kufanya mazungumzo na Atletico Madrid ambapo mwandishi wa habari na mchambuzi maarufu wa soka nchini Hispania Guillaume Balague alithibitisha uwepo wa taarifa hizo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter ambapo aliongeza kuwa United wameanza kulipa fedha za awali kwa ajili ya mshambuliaji huyo.
.
.
Man U tayari ina washambuliaji wanne ambao ni Robin Van Persie,Wayne Rooney, Javier Hernandez Chicharito na Danny Welbeck huku mshambuliaji mwingine Angelo Henriquez akiwa kwenye timu ya Wigan Athletic kwa mkopo .

United imehusishwa na usajili wa mshambuliaji wa Borrusia Dortmund raia wa Poland Robert Lewandowski taarifa ambazo zinaendana na tetesi nyingine zinazomhusisha mshambuliaji Wayne Rooney na usajili wa kwenda kwenye klabu ya PSG.

No comments:

Post a Comment