Saturday, April 6, 2013

DK. HARRISON MWAKYEMBE ANOGESHA BONANZA LA WAANDISHI WA HABARI LEADERS LEO


Waziri wa Uchukuzi Dk Harrison Mwakyembe akizungumza na waandishi wa habari katika bonanza la waandishi wa habari lililofanyika kwenye viwanja vya Leaders Kinondoni jijini Dar es salaal leo, ambapo kumefanyika michezo mbalimbali kwa timu shiriki zikitoka katika vyombo mbalimbali vya habari, Dk. Harrison Mwakyembe akiwa kama mgeni rasmi amegawa nishani na vikombe kwa washindi wa bonanza hili linaloandaliwa na chama cha waandishi wa habari za michezo TASWA, Katika hotuba yake kwa wanahabari Mwakyembe amesema  kama kila mtu atataka kugombea uras nani atafanya kazi nyingine? Akaongeza kuwa yeye anajikita zaidi kufanya kazi zake katika wizara anayoitumikia ya Uchukuzi ili kuwatukia watanzania 2 
Waziri Mwakyembe akimvisha nishani mmoja wa wachezaji wakati alipotoa zawadi kwa washindi kutoka kulia ni Katibu Mkuu wa TASWA Amir Mhando na Mkuu wa Uhusiano na Sheria TBL Bw. Steven Kilindo IMG_0001 
Mchezaji wa Bloggers FC Muhidin Sufiani akibebwa juujuu mara baada ya kupachika penati na kifungia timu yake wakati zilipopambana na timu ya chuo cha DSJ na Bloggers FC kushinda kwa penati 3-2 IMG_0002 
Golikipa wa timu ya Bloggers FC Othman Michuzi akinyanyuliwa na mchezaji mwenzake Mroki Mroki mara baada ya timu hiyo kuifunga timu ya DSJ penati 3-2 IMG_0007 
Kikosi cha Bloggers FC kikiwa katika picha ya pamoja IMG_0022Wangenguaji wa bendi ya Extra Bongo wakiwa katika 
Kiongozi wa kundi la Taarab la Jahazi Mzee Yusuf akiwarusha waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali katika bonanza lililofanyika kwenye viwanja vya Leaders jijini Dar es salaam IMG_0081Waandishi wa habari wakidibwilika stejini  IMG_0098 
Hapa ilikuwa ni fullmauno kwa wanahabari IMG_0105 
Huyu naye akatia fora wakati akicheza na Mwamvuli wake IMG_6894 
Kikosi cha Bloggers kabla ya mchezo wa kwanza. IMG_6902 
Blogger John Bukuku wa Fullshangweblog akiwa na Blogger wa Sufianimafotoblog Muhidini Sufiani ambaye pia anaweza UDJ kama anavyoonekana hapa IMG_6932 
Waziri wa Uchukuzi Dk. Harrison Mwakyembe akiwasili katika viwanja vya Leaders katika bonanza la waandishi wa habari linaloandaliwa na TASWA Kulia ni Mkuu wa Uhusiano na Sheria TBL Bw. Steven Kilindo na kushoto ni Mwenyekiti wa chama cha waandishi wa habari za michezo TASWA Juma Pint

No comments:

Post a Comment