Monday, December 3, 2012

YESI KUWAFUNDISHA VIJANA UJASIRIAMALI ILI WAWEZE KUJIAJIRI WENYEWE


Mwenyekiti Mtendaji wa Taasisi isiyokuwa ya Kiserikali inayojishughulisha na uendelezaji wa wajasiriamali vijana Tanzania Bara( YESI) Bw. Denis Maira (kushoto) akiongeza na waandishi wa habari jana mjini Dar es salaam juu ya  kongamano linatarajia kuwakutanisha wajasiriamali  vijana 250 ambalo litaanza tarehe 6 hadi 8 Mwezi huu . Kongamano hilo linatarajiwa kugharimu shilingi milioni 15 .Kulia ni Ofisa Uhusiano wa Benki ya NBC Eddie Mhina.
……………………………………………………
Na  Heka Paul na Shakila Galus – MAELEZO_Dar es ssalam

Taasisi isiyokuwa ya Kiserikali inayojishughulisha na maendeleo ya Vijana (Young Entrepreneurs Support Initiatives –YESI) inatarajiwa kuendesha kongamano la vijana linalolenga kuwahamasisha kujiajiri katika ujasiriamaliili kukuza biashara nchini.

Akiongea na waandishi wa habari jana mjini Dar es salaam Mwenyekiti Mtendaji Denis Maira , alisema kuwa kongamano hilo liwashirikisha vijana 250 wa mjini hapa na linatarajiwa kugharimu shilingi milioni 15 .

Alisema kuwa kongamano hilo pia litatoa fursa kwa kwa vijana kujifunza mbinu za kukuza biashara na kutengeneza ajira kwa vijana wenzao.

Maira aliongeza kuwa kongamano hilo la siku mbili litawakutanisha wadau wa sekta ya ujasiriamali mbalimbali ambao watajadiliana mbinu za kufungua milango ya maendeleo endelevu ambayo itawawezesha vijana wengi kupambana na tatizo la ajira kwa kujiingiza katika ujasiriamali .

“Hili ni kongamano la kitaifa ambalo linalenga kutafuta suluhisho ya changamoto zinazowakabili vijana hasa tatizo sugu la ajira na athari zake kiuchumi na kiusalama” alisema Maira.

Alisema kuwa hatua itawasaidia vijana katika harakati za kupambana na umaskini na hivyo kujipatia kipato na kuendeleza taifa kwa ujumla.

Mwenyekiti huyo alisema kuwa kongamano hilo litatoa fursa kwa vijana watakaohudhuria kujifunza jinsi vijana wa Kitanzania ambao ni wajasiriamali waliofanikiwa kuanzisha na kukuza biashara zao na hatimaye wakatoa ajira kwa watanzania wengine wakiwamo vijana.

Vilevile washiriki watapata fursa ya kubainisha fursa mbalimbali za kijasirimali , masoko ya ndani na nje na jinsi ya kupata mikopo ya kuwawezesha.

No comments:

Post a Comment