Thursday, November 29, 2012

BI ANASTAZIA ANATAKIWA KUKATWA MGUU WAKE WA KUSHOTO


                Bi Annastazia akiwa Katika Kitanda cha Hospital ya Mkoa wa Mara
       Hapa nikimkabidhi mama yake Annastazia sh 10,000 iliyokuwa imetumwa na mamaAbduwel

Natumia nafasi hii kuwashukuru  Watanzania wote walioguswa na Ugonjwa  wa Bi Annastazia ambaye amekuwa akisumbuliwa na Kuvimba kwa Mguu wake wa Kushoto,kuna watu mbalimbali ambao walipiga simu wakielezea kuguswa na hali hiyo lakini wapo wengine walioenda mbali zaidi na kutoa pesa kidogo ambazo zitaweza kumsaidia  Bi Annastazia.

Mpaka sasa tayri kuna watanzania wawili ambao wametoa fedha  ambazo kwanjia moja zitamsaidia Bi Annastazia,kwa vile nilitumia mtandao huu kuwaomba wamsaidie pia napenda kutumia mtandao huu kutoa shukrani lakini pia kuwaomba wengine ambao hawajafanya hivyo kumsaidia Bi Annastazia. 

Waliotoa ni pamoja na 

   1.    Mama Abduweli wa Mamlaka ya banadari Dar es Salaama- Sh 10,000
  2.     Dada Edna Lwanji  kutoka nchini Uingereza –Sh 137,555.30

Pamoja na kupokea fedha hizo leo nimeongea na mama yake Annastazia na kusema kuwa Mtoto wake anatakiwa kupelekwa jijini Mwanza kwaajili ya kukatwa mguu huo kutokana na vpimo vilivyopatikana baada ya kupigwa X ray.

Hivyo basi watanzania tuendelee kumsaidia Annastazia kwani Mpaka sasa Mama yake hana fedha na hana msaada wowote kwani ni Mjane ,kama utahitaji kumsaidia Bi Annastazia kutuma kwa M Pesa katika namba  0756 035 825

No comments:

Post a Comment