Thursday, December 13, 2012

MKAZI WA KONGWA AHUKUMIWA MIAKA 22

Na. Luppy Kung’alo wa Jeshi la Polisi Dodoma


Mahakama ya Wilaya Kongwa Jana ilimuhukumu Bw. Jumanne Hassan  Miaka (22) mkazi ambaye ni  mkazi wa  kijiji cha Liganga, Kata ya Chitego tarafa ya Nzoisa  wilayani humo  kutumikia kifungo cha miaka (30 ) jela na kuchapwa viboko (12) baada ya kumtia hatiani kwa kosa la kubaka mwanafunzi wa darasa la tano. 




Mwandesha mashtaka  Maulid Manu ambaye ni Mkaguzi  wa Polisi (INSPEKTA) aliiambia Mahakama  hiyo kuwa      Bw.  Jumanne Hassan alimbaka binti mwenye umri wa miaka (12) ambaye jina lake limehifadhiwa na ni mwanafunzi wa  darasa la tano  katika shule ya msingi Liganga iliyopo wilayani kongwa.


Mwendesha mashtaka huyo wa Polisi, aliieleza mahakama kwamba  Bw. Jumanne Hassan alitenda kosa hilo kwa kumvizia binti huyo aliyekuwa anatoka kununua mahitaji ya dukani alipokuwa ametumwa kisha kumkamata  mkono na kumvutia katika chumba cha rafiki yake kilichokuwa jirani  na eneo hilo  kisha kumbaka  na kumtishia kwamba akipiga kelele atamuua.


 Alieleza hayo mbele ya mbele ya hakimu  wa mahakama  ya Wilaya ya Kongwa  Bw. Godfrey Pius, aidha alisema tukio hilo lilitokea Novemba moja, mwaka  jana (2011) majira ya sa mbili na nusu usiku katika eneo la kijiji cha Liganga, Kata ya Chitego na  Tarafa  ya Nzoisa Wilayani Kongwa.

No comments:

Post a Comment