MUSOMA
Mlinzi wa kampuni
ya ulinzi ya salama iliyoko manispaa ya musoma Mkoani Mara ameuwawa kikatili
kwa kuchinjwa shingo akiwa lindo katika Pub inayojulikana kwa jina la Tulivu na
watu hao Wanaosadikika kuwa ni Majambazi kuondoka na crate mbili za bia na viti
.
Taarifa ya
kamanda wa polisi wa mkoa wa Mara kamishina msaidizi Mwandamizi wa Jeshi hilo Absalom mwakyoma
alisema kuwa majira ya asubuhi eneo la barabara ya majita kata ya kamunyonge
manispaa ya Musoma uligunduliwa mwili wa John Nyanganya ( 22) mlinzi wa kampuni ya salama security
ukiwa umekatwa shingo .
Taarifa hiyo
imeendelea kusema kuw uchunguzi umeonyesha kwamba wauaji hao
walivunja pub hiyo ,baada ya kumuua na kuiba crate
mbili za bia na viti vya plastiki saba
venye thamani ya shilingi laki
moja na elfu sabini.
Katika taarifa
hiyo ya Kamanda Mwakyoma alisema kuwa ufuatiliaji wa kina unafanyika
katika kuwabaini wahalifu hao waliofanya unyama huo ili wafikishwe
kwenye vyombo vya sheria.
Kufuatia hali
hiyo mpaka sasa Mtu mmoja anashikiliwa
na jeshi la polisi Mkoani hapa akiwa na nondoo tatu ,mtarimbo pinde na mishale
mitatu ,kirungu na nguo za kike ambapo insemekana kuwa Wahalifu hao walivaa
nguo za kike kuficha sura zao.
No comments:
Post a Comment