Monday, November 26, 2012

MAANA YA a.k.a YANGU



Jina langu halisi naitwa Edwin Harrison Moshi ni mtangazaji kwenye kituo cha redio Kiitwacho Kitulo Fm kilichopo wilayani Makete katika mkoa mpya wa Njombe
 
Nimeamua kukutumia habari hii kutokana na mashabiki wangu wengi kuniuliza maana ya a.k.a yangu
 
A.k.a yangu ni Eddy Mo Blaze ambayo nilianza rasmi kuitumia mwaka 2007 nilipoanza rasmi masuala ya utangazaji wa redio, Mwanzoni nilikuwa nikijiita Eddy Mo ikiwa ni kifupi cha Edwin Moshi lakini baadaye baada ya mwalimu wangu wa studio kunifundisha masuala ya u-dj, niliweza kufanya hiyo kazi kwa kiasi kikubwa na kwa kiwango zaidi ya alivyokuwa akitegemea na ndiyo akaniongezea jina la Blaze kwenye aka yangu akimaanisha niliweza kuwablaze watu(kuwadatisha), hivyo badala ya kuwa eddy mo ikawa Eddy Mo Blaze
 
Kwa hiyo Eddy Mo ni kifupi cha majina yangu Edwin Moshi na Blaze ni kinogesho nilichopewa na mwalimu wangu, Kwa kifupi mashabiki wangu hiyo ndiyo maana ya Eddy Mo Blaze

No comments:

Post a Comment