Promotions Manager wa EBONY FM Bonny Zacharia Nyatogo (aliyekaa kulia) akijiweka sawa tayari kwa uzinduzi wa Tamasha la Mtikisiko hewani |
Timu nzima ya watangazaji wa Radio Ebony Fm wakiwa studio katika uzinduzi wa Mtikisiko 2012
Radio Ebony FM yenye makao yake makuu mkoani Iringa na inayorusha matangazo yake katika masafa ya 87.8 (Iringa), 88.2 (Makambako), 94.7 (Mbeya), 91.6 (Dodoma), 95.4 (Morogoro) na 102.2 (Songea) Oct 01 kupitia kipindi chake cha mchana "THE SPLASH" imezindua hewani (on air launching) TAMASHA lake kubwa la kila mwaka maarufu kwa jina la "MTIKISIKO" ambalo linatarajiwa kuanza katikati ya mwezi huu na kupita karibu sehemu zote inaposikika redio hiyo.
Akizungumza katika uzinduzi huo Promotions Manager wa EBONY FM
Bonny Zacharia Nyatogo amesema, mwaka huu EBONY FM ikishirikiana na
kampuni mama ya burudani EBONY ENTERTAINMENT wamejipanga vya kutosha
kukata kiu ya burudani kwa wapenda burudani wote kwenye mikoa ya Nyanda
Za Juu Kusini ambayo wana uhakika haijakatwa bado.
Mratibu mkuu ni Eddo Bashir kama ilivyo kwa miaka iliyopita, naye
amesema maandilizi ya TAMASHA hilo yameshaanza na muda wowote kuanzia
sasa ratiba rasmi itatangazwa hasa tarehe na maeneo TAMASHA hilo
litakapopita. Kauli mbiu ya TAMASHA hilo mwaka huu ni "Ndo Vileee..!!!"
Tamasha la "MTIKISIKO" kihistoria lilianza mwaka 2007 wakati huo
likiitwa "PAMOJA TIME" ambapo mwaka 2008 lilibadilishwa jina na kuanza
rasmi kuitwa "MTIKISIKO"...nia na madhumuni ya TAMASHA la "MTIKISIKO" ni
kukutana pamoja na wasikilizaji wa ukweli wa EBONY FM na kurudisha kwao
LOVE wanayotoa kwa redio.
No comments:
Post a Comment