Wito umetolewa kwa Jamii kuwapenda,kuwaheshimu na
kuwathamini watu wenye Ulemavu ikiwemo kuheshimu haki zao na kuwasaidia pale
wanapohitaji msaada.
Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Asasi ya Lake
Victoria Disability Center (LVDC) Bw. Dennis Maina inayojihusisha na watu wenye
ulemavu mkoani Mara.
Amesema Asasi yao imenufaika na ruzuku iliyotolewa
na Taasisi ya The Foundation for Civil Society ya jijini Dar es Salaama kwa
Mwaka 2011-2012 ambapo asasi hiyo ilipata kiasi cha Shilingi milioni arobaini
na nne laki tisa na elfu sitin na sita na mia saba (44,966,700) katika
kutekeleza mradi wa Kuwajengea uwezo watu wenye ulemavu na wadau katika mambo
ya Ulemavu.
Bw Dennis amesema kuwa toka wameanza kutekeleza
mradi huo uliofadhiliwa na Taasisi ya Foundation for Civil Society ya jijini
Dar es Salaama kwa Mwaka 2011-2012 wamepata faida kubwa ikiwemo kuwajengea
uwezo wa kutoa elimu kwa watu wenye ulemavu,huku uwelewa katika jamii kuhusiana
na mambo ya watu wenye ulemavu kuongezeka na hivyo kutambua haki zao za msingi.
Mbali na hizo lakini pia amesema faida nyingine ni
pamoja na Walemavu kuelewa haki zao huku Mahusiano yakionekana kuwa mazuri kati
ya Jamii na Watu wenye Ulemavu.Katika kutekeleza mradi huo Bw Dennis amesema
kuwa kituo chake kimenufaika na ununuzi wa Vifaa kutokana na ruzuku waliyoipata
kutoka Taasisi hiyo pamoja na mradi huo kukamilika.
Ameongeza kuwa faida nyingine ambayo Kituo chake
kimepata ni pamoja na kuaminika katika Jamii kutokanma na kujitoa kusaidia
Jamii ya watu wenye Ulemavu Mkoani Mara.
Akiongelea mabadiliko yaliyoonekana kutokana na
kutekeleza Mradi huo,Mkurugenzi huyo wa LVDC amesema mabadiliko makubwa ni
kushamiri kwa mahusiano kati ya watu wenye Ulemavu na wale wasio Walemavu
tofauti na ilivyokuwa Mwanzo,watoto wenye Ulemavu kupelekwa Shule huku awali
walionekana kutothaminiwa katika masuala ya elimu.
Mabadiliko mengine amesema kuwa ni pamoja na Watu
wenye Ulemavu kupewa kipaumbele katika masuala ya Matibabu tofauti na
ilivyokuwa awali huku Semina na Warsha
zikionekana kuwasaidia Viongozi katika kutambua haki za watu wenye Ulemavu na
Mahitaji yao
Aidha kuhusu kushirikishwa Jamii katika mradi huu ni
pamoja na wahuska wa Mradi kuchagua Shule moja kila wilaya mkoani Mara na
kufanya nazo kazi hasa lengo likiwa ni kufikisha ujumbe kwa Jamii kuhusu
Masuala ya Walemavu.
Mbali na kufanya kazi za kusaidia watu wenye Ulemavu
pia Mkurugenzi huyo amesema kuwa waliweza kuendesha Vipindi 45 vya redio
(Victoria Fm) ambapo walitumia nafasi hiyo kutoa elimu kuhusiana na Watu wenye
Ulemavu huku baadhi ya watu wakipiga simu na kuuliza maswali na kasha kupata
ufafanuzi kutoka kwa wataalam wa Masuala ya watu wenye Ulemavu.
Kwa kuelewa ukubwa wa Tatizo la Walemavu katika
Jamii Mkurugenzi huyo amesema kuwa asasi yake inaandaa mkakati wa kutanua wigo
wa kuzifikia haki za watu wenye Ulemavu katika mkoa wa Mara umeandaliwa ifikapo
Desemba 2012.
Bw. Dennis amesema kuwa kulingana
na Takimu zilizokusanywa na LVDC
mwaka 2010 kwa watu 3600 wenye ulemavu mkoa wa Mara wakati asai hiyo inaendesha
mafunzo ya upigaji kura kwa watu wenye ulemavu yaliyokuwa yamefadhiliwa na UNDP
na DELLOITE iligundulika kuwa hakuna
mkakati wala mpango kazi ulioandaliwa na
Viongozi wa vyama vya watu wenye Ulemavu .
Katika hatua nyingene Mkurugenzi huyo amesema kuwa
asasi yake ina mahusiano chanya na baadhi ya Taasisi hapa nchini na nje ya nchi
na ndiyo maana imekuwa ikipata ufadhili katika miradi mbalimbali wanayoiandaa.
Mkurugenzi huyo wa LVDC amesema kuwa pamoja na
kuonekana kufanikisha mradi huo vizuri kwa asilimi kubwa lakini bado kumekuwepo
na changamoto mbalimbali ambazo zilionekana kuwa kikwazo katika kukamilisha
mradi huo ikiwemo pamoja na Jamii kutowathamini watu wenye Ulemavu,asilimia
kubwa ya watu wenye ulemavu hawajapata elimu ya awali huku baadhi ya wanajamii
wakiendeleza Mila Potofu kwa watu wenye ulemavu katika Familia.
Pamoja na changamoto hizo lakini changamoto zingine
ni pamoja na Jamii kutokubali kubadilika katika kuwatambua watu wenye Ulemavu kama
watu wengine,kuboresha huduma zinazowahusu watu wenye Ulemavu kutokana na
Mazingira yao kutokuwa rafiki.
Bw Dennis Maina alisema kuwa Changamoto zingine ni
pamoja na Uwelewa wa watu wenye Ulemavu kuwa mdogo na kuona kile wanachofanyiwa
ni sawa huku baadhi ya watu wakiona ni kupoteza muda kumshughulikia mtu mweye
Ulemavu na wengine wakiendelea kuwa na mtazamo hasi pamoja na suala la Umaskini
katika Jamii pia imeonekana kuwa Changamoto.
Wakiongelea kuhusu faida walizozipata kutokana na
mradi huo uliokuwa ukitekelezwa na LVDC kwa ufadhili wa Taasisi ya The
Foundation for Civil Society ya jijini Dar es Salaama kwa Mwaka
2011-2012,baadhi ya walengwa wamesema kuwa wamenufaika kwa asilimia kuwa na
mradi huo huku wakiomba asasi hiyo kuendelea kuwasaidia hata baada ya Mradi huo
kuwa umekamilika.
Kambarage Madaraka mtoto anayesoma darasa la tatu
katika Shule ya Msingi Kigera ambaye ana ulemavu wa Miguu amesema kuwa kwa
asilimia kuwa amenufaika na mradi huo kutokana na Mafunzo waliyoyapata nay eye
kufahamu haki zake kama Mlemavu.
Mbali na Kambarage pia baadhi ya wanafunzi ambao
walihusishwa katika Mradi huo wamesema kuwa wamenufaika kwa kupata elimu
inayohusiana na Masuala la walemavu lakini wakalaani baadhi ya watu ambao bado
wanaendelea kuwatenga watu wenye Ulemavu na kuwanyima haki zao za msingi.
Naye Mwalimu Christina Stephen kutoka Shule ya
Msingi Kigera A ambaye hujihusisha na masuala ya Watu wenye Ulemavu shuleni
hapo amesema kuwa katika mradi huo amenufaika kutoka na kujua haki za
Walemavu,kuwapenda na kuwathamini kama watu wengine.
Katika Shule ya Msingi Nyabange iliyopo wilaya ya
Butiama ambapo mradi huu pia umefika umeweza kuwanufaisha zaidi ya Vijana 10
kutoka shuleni hapo huku wengi wao wakisema kuwa wamejifunza mambo mbalimbali
yanayohusiana na Masuala ya watu wenye Ulemavu.
Walisema kuwa wamejua haki za Walemavu,kutambua
Walemavu,kutowatenga Walemavu,kuwapa haki sawa Walemavu,kuwasaidia
Walemavu,kuwapa elimu na Makazi bora watu wenye Ulemavu.
Rajabu Josephat mtoto anayesoma darasa la nne katika shule hiyo ambaye anaulemavu wa miguu
yote miwili amesema kuwa m Taasisi ya The Foundation for Civil Society ya
jijini Dar es Salaama kwa Mwaka 2011-2012 umemnufaisha ikiwa pamoja na
kusaidiwa baiskeli ambayo imeweza kumrahisishia shughuli zake pamoja na kujua
haki zake kama Mlemavu.
Nao Viongozi wa Serikali wakiongelea Mradi huo
wamesema kuwa wanaishukuru LVDC na Taasisi ya The Foundation for Civil Society
ya jijini Dar es Salaam kwa kufanikisha Mradi huo katika Jamii ya Mkoa wa Mara.
Bw Mfungo Bunini Mtendaji wa Kata ya Mkendo ambapo
mradi huo pia umeweza kunufaisha baadhi ya vijana amesema kuwa kujitokeza kwa
Taasisi kama The Foundation for Civil Society ni msaada mkubwa kwa Serikali
kwani serikali haiwezi kufikia watu wote kwa wakati lakini taasisi kama hizo zinapokuwepo
zinasaidia sana katika Jamii
“Mimi napenda
sana kuishukuru hii Taasisi iliyowafadhili hawa jamaa kwani inasaidia Serikali
yetu ambayo ina mambo mengi katika Jamii na pia napenda watu wengine wajitokeze
kusaidia kama ilivyo taasisi ya The Foundation for Civil Society” alisema
Mtendaji huyo
Katika kuufanikisha mradi huo Bw Dennis amesema kuwa
ingekuwa kazi ngumu kama wasingeweza kushirikiana na baadhi ya Sekta mkoani
Mara kufanikisha zoezi hilo,kwasababu hiyo alisema kuwa wameweza kutoa majalida
mbalimbali ambayo yaekuwa yakielezea malengo ya Asasi hiyo na lengo la mradi
huo ambapo wanajamii walielewa na kuto ushirikiano.
Mbali na hivyo ameongeza kuwa kumekuwepo na semina
za Mara kwa Mara kwa wanajamii zinazohusiana na Masuala ya Walemavu hivyo kwao
ilikuwa rahisi kufanikisha mradi huo.
“Unajua kama
tusingeshirikisha jamii inayotuzunguka ingekuwa kazi maana jamii hiyo hiyo bado
ilikuwa na Mtazamo tofauti katika mambo yanayohusu Walemavu hivyo tukaona
kwanza tuwape vitu ambavyo watakuwa wanasoma ikiwa ni njia ya kuzielewa haki za
walemavu lakini pia kuwashirikisha katika Semina mbalimbali tunazoziandaa”
alisema Bw Dennis
Akiongelea ufadhili walioupata kutoka The Foundation
for Civil Society,Mkurugenzi huyo alisema kuwa wafanyakazi wote wa asasi yake
wamekuwa na ufahamu mkubwa kuhusu masuala ya watu wenye ulemavu,kupata uwezo wa
kuwahudumia watu wenye Ulemavu tofauti na awali,wameweza pia kujua haki za watu
wenye Ulemavu na pia wameweza kupata elimu jinsi ya kutekeleza Mradi kwa
ufanisi.
Mbali na kuongelea ufadhili huo,Mkurugenzi huyo
ameishukuru Taasisi ya The Foundation for Civil Society kwa ruzuku waliyoipata
kwani kwa asilimia kuwa imeweza kusaidia kubadilisha Maisha ya watu wenye
Ulemavu kimtazamo na Kimaisha Mkoani Mara.
No comments:
Post a Comment