Wednesday, October 24, 2012

BARABARA ZANZIBAR KUFUNGWA


Na Mwanshi wa Jeshi la Polisi Zanzibar

Jeshi la Polisi zanzibar limetangaza kuzifunga baadhi ya barabara za mji wa Zanzibar ili kuwawezesha wananchi wakiwemo watoto wadogo kusherehekea siku kuu ya Eddi el Haji kwa usalama na amani.

Afisa Habari Mkuu wa Jeshi la Polisi Zanzibar Inspekta Mohammed Mhina, amezitaja baadhi ya barabara zitakazofungwa kwa muda wa siku nne kuanzia Ijumaa wiki hii hadi Jumatatu wiki ijayo kuwa ni ile inayotoka Mnazi Mmoja hadi Viwanja vya michezo vya Maisala, barabara ya kutoka Ofisi ya Baraza la Wawakilishi la Zamani kuelekea Viwanja vya Maisala na Barabara ya ya kutoka Ukumbi wa CCM kuelekea Mnazi Mmoja.

inspekta Mhina, amesma kuwa barabar hizo zitafungwa kuanzia majira ya saa 9.00 arasili hadi saa 4.30 usiku kwa kila siku muda ambao watu wengi watakuwa wamesharejea majumbani kwao baada ya kusherehekea siku hiyo.

Awali akitoa taarifa kwa vyombo vya habari mjini Zanzibar, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Ungauja ACP Aziz Juma Mohammed, alisema kuwa sherehe hizo zitaadhimishwa kwa muda wa siku nne mfululizo zitaanza Ijumaa ya Oktoba 26 hadi Jumatatu ya Oktoba 29 2012.

Katika hatua nyingine Kamanda Aziiz amesema Jeshi la Polisi mkoani humo litaweka vituo vidogo vya Polisi katika maeneo yote ya viwanja vikubwa vitakavyokuwa na mikusanyiko mikubwa ya watu kwa lengo la kuwahakikishia wananchi ulinzi wa usalama wao pamoja na mali kwa wakati wote wa sherehe hiyo.

Kamanda huyuo amevitaja viwanja vitakavyokuwa na mikusanyiko mikubwa kwa ajili ya sherehe hizo za Eddi El Haji  kuwa ni Mnazi Mmoja, uwanja wa Demoklasia, Jamhuri Garden, Forodhan Park, Kiembe Samaki, Nyarugusu, Maungani na Bububu Meli nne.

Kamanda Aziz amesema Kiwanja cha michezo cha Kariakoo mjini Zanzibar kwa mara nyingi hakitaweza kutumika kutokana na kuharibika.
  
Amewataka waqzazi na walezi kutowapa vijana wao makundi makubwa ya watoto wadogo ili kuepuka kupoteana katika viwanja hivyo ambavyo mara nyingi vinakuwa na umati mkubwa wa watu.

Amewakumbusha wazazi na walezi hao pia kutowaruhusu watoto wao kwenda karika fukwe za bahari kuogelea pasipo uwangalizi wa watu wazima kwani amesema kuwa uzoefu unaonyesha kuwa watoto huzama na kufa maji baharini pasipokuwa na uwangalizi katika nyakati za siku kuu kama hizi.

Hata hivyo Kamanda Aziz amewataka wazazi kuwaelimisha watoto wao kuwa wanapobaini kupotezana na ndugu na jamaa zao wafike katika vituo hivyo vidogo vya Polisi na yeyote atakayepotelewa aweze kufika hapo kwa utambuzi na kumpata mtoto wake.

Amewakumbusha wananchi kutoziacha nyumba na sehemu zao za biashara pasipo na uwangalizi wa kutosha wanapotoka kwenda katika viwanja vya burudani ili kuepuka kuwapa wezi fursa ya kupora mali zao.

Kwa upande wa madereva kamanda aziz amewataka madereva wote kuendesha vyombo vyao kwa mwendo wa kadri na kuepuka kuvunja sheria, taratibu na kanuni za usalama barabarani na kwamba kwa yeyote atakayekaigi agizo hilo hatua kazi zitachukuliwa dhidi yake ikiwa ni pamoja na kukamatwa na kufikishwa mahakamani.

Visiwani Zanzibar sherehe za Eddi El Fitri na Iddi El haji ndizo sherehe kuwa kupita zote za kiserikali na husherehekewa kwa muda wa siku nne mfululizo katika viwanja mbalimbali ingawa utaratibu huo wa kusherehekea hauingiliani na na ule uliopo kwenye kalenda ya Serikali.

Mwisho

VITAMBULISHO VYA TAIFA

Na Mohammed Mhina, Zanzibar 
Zaiidi ya aslimia 80 ya wakazi wa wilaya ya Kusini Unguja Zanzibar wamejitokeza kujiandikisha kupata vitambulisho vya Taifa wengi wao wakiwa ni vijana.

Mkurugenzi wa Vitambulivyo vya Taifa Zanzibar Bw. Vuai Mussa Suleiman, amesema kuwa zoezi hilo lililoanza mwanzoni mwa mwezi huu  limeonyesha mafanikio na Jumatatu ijayo ya Oktoba 29, 2012 zoezi hilo litaingia katika wilaya ya Kati katika mkoa huo wa Kusini Unguja.

Bw. Vuai alikuwa akitoa taarifa kwa Waandishi wa Habari aliofuatananao katika ziara ya pamoja ya kuvitembelea vituo hivyo vya kujiandikishia katika wilaya ya Kusini unguja zoezi ambalo lilianza Oktoba 15, mwaka huu na linatarajiwa kumalizika kesho Alhamisi Oktoba 26, 2012.

Bw. Vuai amewataka wananchi wa wilaya zingine kujiandaa kwa kupiga kopi baadhi ya vielelezo muhimu vikiwemo vitambulisho na vyeti vya kuzaliwa ili kurahisisha utekelezaji wa zoezi hilo.

Wakati wa ziara hiyo baadhi ya wasimamizi na masheha waliopo katika vituo hivyo wameelezea mafanikio na changamoto zinazojitokeza ambapo wamesema baadhi ya watu wanaofika kujiandikisha hawaelewi hata maana na foto kopi.

Msimamizi wa Kituo cha Bwejuu Bw. Khamisi Mabrouk Mbaraka,baadhi ya watu wanaofika katika vituo vyao wanapeleka hati halisi pasipo na kopi. 

Nao baadhi ya Mashehe wamesema kuwa hakuna uwezekano wa mtu asiyehusika kujipenyeza na kujiandikisha kwa sababu watu wote wakiwemo wasio na vitambulisho vya Uzanzibar Mkazi wanaoshi katika shehia zao wameorodheshwa majina na kwamba ikijitokeza utata Sheha anawajibika kulitatua kwa kupitia kumbukumbu za wakazi wa eneo lake.

Akizungumza katika kituo cha Bwejuu, mmoja ya watu waliofika kujiandikisha Bi. Mwakito Mkadamu, ameelezea umuhimu wa vitambulisho hivyo kwa jinsi alivyoelimishwa kupitia vyombo vya habari na kusema kuwa kinaweza kumsaidia katika masuala mbalimbali yakiwemo ya kifamilia na kiuchumi.

Miongoni mwa watui wanaojiandikisha kupata vitambulisho hivyo wapo wa kutoka katika mikoa mbalimbali ya Tanzania bara wanaoishi Zanzibar kwa shughuli binafsi na za kikazi.

No comments:

Post a Comment