Na Mohammed Mhina, wa Jeshi la Polisi zanzibar
Askari
Polisi mmoja wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia Ziwani Mjini Zanzibar
ameuawa kwa kukatwakatwa mapanga na watu wanasadikiwa kuwa ni wafuasi wa
Jumuiya ya Uamsho.
Kamishna
wa Polisi Zanzibar CP mussa Ali Mussa, amemtaja askari aliyeuawa kuwa
ni mwenye namba F.2501 CPL Saidi Abdrahamani Juma(41) ambaye aliuawa saa
6.30 usiku wa kuamkia leo wakati akiwa njiani kurejea nyumbani baada ya
kumaliza zamu yake ya kazi.
Katika
hatua nyingine Kamishna Mussa amesema watu kumi wanashikiliwa na Polisi
kwa tuhuma za kufanya fujo na vurugu zilizopelekea uharibifu mkubwa wa
barabara kwa kuchoma matairi na kuweka mawe barabarani.
Amesema
na misako mbali mbali imeanzishwa kuwakamata wale wote waliofanya
mauaji ya CPL Said Abdulrahman. Tuelewe kuwa aliyeuliwa ni askari
Polisi, ni raia wa Tanzania na ni muumini wa dini ni lazima tuhakikishe
waliofanya unyama huu wanakamatwa na kufikishwa Mahakamani kama Sheria
za nchi zinavyotuelekeza.
Amesema
kuuawa kwa askari huyo kunafuatia fujo na vurugu za wafuasi wa Jumuiya
hiyo ya uamsho Sheikhe Faridi ambapo amesema hadi sasa watu kumi wamekamatwa kwa tuhuma za makosa mbali mbali yaliyotokana na vurugu hizo.
Kamishna Mussa amesema upelelezi wa kujua ukweli juu ya uvumi wa kutekwa kwa Sheikh Farid bado unaendelea.
Amesema
kuwa jana majira ya saa 6:30 za mchana Sheikh Mselem alifika katika
kituo cha Polisi Madema mkoa wa Mjini Magharibi na kutoa taarifa za
kupotea kusikojulikana kwa Bw. Faridi.
Akimkariri
mmoja wa Viongozi wa Uamsho, Kamishna Mussa amesema Bw. Faridi ambaye
hadi sasa hajulikani aliko akipotea tangu tarehe 16,10,2012.
“Taarifa
zilizoripotiwa polisi madema ni kuwa kuwa Kiongozi mwenzao wa Jumuiya
ya UAMSHO Sheikh Farid ametekwa na hawamuoni tokea jioni ya tarehe
16.10.2012” Alisema kamishna Mussa.
Amesema
baada ya taarifa hiyo Polisi walianza uchunguzi kwa kuwahoji watu
mbalimbali walio karibu na Bw. Faridi ambapo amesema waliohojiwa ni
pamoja na dereva wa Bw. Farid Bw. Said Omar Said.
Kamisna
Mussa amesema kwa mujibu wa dereva wa gari ya Sheikh Farid, yeye
alimuacha eneo la Mazizini baada ya kununua umeme na ni farid mwenyewe
aliyemtuma dereva wake kupeleka umeme nyumbani wakati yeye Sheikh Farid
akizungumza na watu wengine waliokuwemo kwenye gari moja aina ya NOAH
ambayo namba zake hazikupatikana.
Amesema
dereva huyo aliporudi tena katika eneo alipokuwa amemuacha Bw. Faridi
hakumkuta na ndipo alipotoa taarifa kwa viongozi wengine wa Jumuiya
hiyo.
Amesema
wakati taarifa hizo zikipelekwa kuripotiwa Polisi wakati huo wafuasi wa
Jumuiya ya UAMSHO walijikusanya katika msikiti wa Mbuyuni na kuanzisha
fujo kwa kuanza kuchoma moto kwenye jaa la karibu na msikiti huo. Baadae
fujo zilienea haraka katika maeneo mbali mbali ya mjini kwa kufanyika
uharibifu mbali mbali wa mali za Serikali, Chama tawala na za wananchi
kwa ujumla.
Mbali
ya hofu kubwa kwa wananchi juu ya maisha na mali zao, fujo hizi
zilileta hasira ya kuchoma na kuharibu miundo mbinu ya barabara,
kuharibu maskani za Chama tawala CCM za Kisonge na muembeladu kwa
kuzichoma moto. Gari moja ya Serikali ilivunjwa kioo kidogo cha pembeni,
gari ya zimamoto kuvunjwa kioo cha mbele. Aidha walivunja duka la Pombe
na kuiba mali iliyokuwemo ndani.
Kamisha
wa Polisi Zanzibar ameendelea kuwaomba wananchi kudumisha amani na
utulivu katika maeneo yao, kutupa taarifa za watu waliohusika na vurugu
pamoja na mauaji ya askari wetu. Tuendelee kukumbushana kutii Sheria
bila ya shuruti.
No comments:
Post a Comment