MUSOMA
MAHAKAMA ya Hakimu mkazi mkoa wa
Mara Leo Imetoa hukumu ya kesi ya jinai namba 360 ya mwaka 2010 iiliyokuwa ikiwahusu
watuhumiwa sita.
Watuhumiwa hao sita wanadaiwa
kumteka na kumshambulia vibaya aliyekuwa Mwenyekiti wa chama cha Wananchi CUF
wilaya ya Musoma mkoani Mara Bw Didi Musira Koko.
Bw Didi Musira Koko akiwa hospital baada ya kushambuliwa Mwaka 2010
Katika tukio hilo la kushambuliwa
kwa Bw Didi Musira Koko aliyekuwa Mwenyeki wa CUF Manispaa ya Musoma mkoani
Mara ilisababisha kuumia mguu ambapo kwa
mujibu wa taarifa za kitabibu ilionekana kuwa mfupa umehama lakini
haukuvunjika.
Watuhumiwa katika kesi hiyo walikuwa ni Bw Mapinguzi Muhere,Magori Zembwera na Geofrey Marwa.Wengine ni Justine
Dida ,Dickson Anthony na Manumbu Magacha ambapo Mahakama iliwaachia huru watu
watano waliokuwa katika kesi hiyo huku Bw Mapinduzi Mhere akikutwa na hatia
Hukumu hiyo iliyosomwa na Hakimu wa Mahakama ya
Hakimu mkazi mkoa wa Mara Hussen Mushi
ilitoa adhabu kwa Bw Mapinduzi Mhere kifungo cha Mwaka mmoja Jela au kulipa Faini
ya Shilingi laki Tatu
Tukio hilo lililotokea Septemba 25
Mwaka 2010,lilitokea wakati Didi Musira koko akitoka katika mkutano wa kampeni
wa aliyekuwa mgombea urais kupitia chama chama Mapinduzi CCM Rais Jakaya
Kikwete katika uwanja wa shule ya msingi Mukendo.
No comments:
Post a Comment