Musoma,
AJALI ya gari iliyotokea jana jioni katika Kijiji cha Mkiringo Wilaya ya Butiama Mkoani Mara ikiwa safarini kutoka Musoma Kuelekea Nyamswa wilaya ya Butiama Mkoani Mara
imeuwa Watu 13 na 14 kujeruhiwa.
Wakiongea na Tanzania daima mashuhuda wa ajali hiyo iliyohusisha gari aina ya Toyota Hiace lenye namba T123 CAE iliyokuwa ikiendeshwa na dereva aliyefahamika kwa jina la Emmanuel Joseph maarufu kama Diouf ilikuwa katika mwendo kasi huku ikiwa imebeba abiria kupita kiasi waliokuwa katika safari hiyo.
Mashuhuda walisema gari hilo likiwa katika mwendo kasi lilipasuka tairi la nyuma upande wa kulia na kupinduka mara tatu na kupelekea vifo pamoja na majeruhi hao waliolazwa na kuhifadhiwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mara.
Kwa mujibu wa maelezo ya Mganga mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Mara Dk. Samson Wenani alisema kuwa amepokea majeruhi pamoja na maiti waliohifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti katika Hospitali hiyo.
Dk. Wenani aliwataja waliofariki ni watu 12 ambao walitambuliwa na ndugu zao huku mmoja akiwa bado hajatambuliwa kuwa ni dereva wa gari hilo Emmanuel Joseph,Pendo John (39) pamoja na mtoto wake Joseph Richard (5) wakazi wa Bisarye,Razak Shaabani,Hamis Kanyoro,Nyamazore John,Innocent Fares Kweka na Jiadhari Saidi Dogori wakazi wa Nyamswa.
Wengine waliotajwa kufariki katika ajali hiyo ni Makuli Maguri,Aizaki Hassan, pamoja na watu wengine wawili waliotambulika kwa jina moja moja la Masoke na Richard ambao ni wakazi wa Wilayani Butiama.
Aliwataja majeruhi katika ajali hiyo wanaoendelea kupata matibabu huku hali zao zikiendelea kuimarika kuwa ni Nyamakunguru Fanuel,Nyamazege Warioba,Gosbert Waryoba,Hamisi Wisaka,Hamisi Gibombi na Hamis Nyaga.
Alisema wengine waliojeruhiwa katika ajali hiyo na kulazwa katika Hospitali hiyo ni pamoja na Mganda Nyamajege,Efrancia Kiamanzi pamoja na Beatrice Siriwa ambao ni wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Chief Ihunyo waliokuwa wakitokea Jijini Dar es salaam kuelekea shuleni.
Majeruhi wengine ni pamoja na Mwalimu wa shule ya msingi Butiama Betreace Komba ambaye amevunjika sehemu ya juu ya mguu wake wa kulia,Bunuli Madube pamoja na mtoto wa miaka nane Matha Makuli ambaye baba yake waliyekuwa naye katika ajali hiyo alifariki Dunia.
No comments:
Post a Comment