Saturday, July 28, 2012

MKUU WA MKOA WA MWANZA AFUNGUA MAFUNZO YA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2012 KWA WAANDISHI WA HABARI KANDA YA ZIWA, NA KATI 

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Evarist Ndikiro.

Baadhi ya waandishi wa Habari wakimsikiliza mgeni rasmi
   Afisa Uhamasishaji Said Ameir akitoa Maelezo juu ya Sensa kwa waandishi wa Habari

SENSA-MWANZA


SERIKALI imesema kuwa haitamvumilia mtu yeyote atakayeingiza sula la itikadi za kisiasa na imani za kidini katika zoezi la sensa na makazi linalotarajia kuanza Augost 26 mwaka huu.



Akifungua semina ya siku mbili kwa waandishi wa habari kutoka mikoa kumi ya kanda ya ziwa na kanda ya kati,mkuu wa mkoa wa Mwanza Injinia Everist Ndikilo amesema kuwa vyombo vya habari vinajukumu kubwa katika kufanikisha zoezi la Sensa na makazi linafanikiwa.



Amesema jukumu kubwa la vyombo vya habari katika zoezi la Sensa ni kuelimisha,kuhabarisha na kuhamasisha wananchi kujitokeza katika zoezi hilo litakapoanza.



Injia Ndikilo amesema kuwa taarifa zote zitakazopatikana katika zoezi hilo zitakuwa siri huku akisema kuwa zoezi hilo halitahathiri shughuli za kiuchumi.



Awali akimkaribisha mgeni rasmi katika semina hiyo, Afisa uhamasishaji Said Ameir  amesema kuwa sekta ya habari ni miongoni mwa wadau wakubwa katika zoezi la Sensa huku akisema kuwa Tanzania ni moja ya nchi inayofanya zoezi la Sensa kwa ubora.



Zoezi la Sensa na Makazi linatarajiwa  kufanyika Agost 26 huku wananchi wakihimizwa kuwa zoezi hilo ndilo litasaidia katika mipango ya Maendeleo hapa nchini.


No comments:

Post a Comment