Tuesday, July 31, 2012

MATUKIO KATIKA KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI MJINI MUSOMA



Mstahiki Meya wa Manispaa ya Musoma Alex Kisurura kulia akiwa na Makamu wa
MGOMO WA WALIMU HAUUSIANI NA MADAI YA NYUMA

Na Shomari Binda
Musoma,


Suala la mgomo wa walimu ulioanza jana Nchi nzima umedaiwa hauusiani na walimu hao kudai madai ya madeni ya malimbikizo mbalimbali ya miaka ya nyuma bali yapo masuala mengine ambayo yalipelekea kuwepo kwa mgomo huo.

Kauli hiyo ilitolewa na kaimu mkurugenzi wa Manispaa ya Musoma John Masero alipokuwa akijibu swali la diwani wa kata ya Nyakato (CCM) ambaye pia ni kiongozi wa kambi ya Upinzani katika kikao cha Baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Halimashauri ya Manispaa ya Musoma.

Katika swali lake la msingi katika kuchangia taarifa ya utekelezaji ya mwaka 2011-2012,Diwani huyo alitaka kujua sababu zilizopelekea walimu kuingia katika mgomo ikiwa Halimashauri hiyo haina deni lolote wanalodaiwa na walimu.

Akimjibu Diwani huyo, Masero alisema walimu wamegoma kutokana na madai ya nyongeza ya mishahara kwa asilimia 100,nyongeza ya asilimia 55 kwa walimu wanaofundisha masomo ya sayansi na hisabati pamoja na nyongezailimia 30 kwa walimu wanaofundisha katika mazingira magumu.

Alidai Halimashauri ya Manispaa ya Musoma ilifanyia kazi agizo la Serikali katika kuhakiki madai ya walimu nakuwalipa na kufikia hivi sasa hakuna mwalimu yeyote anayehidai Manispaa hiyo malimbikizo ya madai ya nyuma.

Alisema kwa sasa hakuna utaratibu wowote wa kufanya uhamisho kwa walimu kama hakuna fedha za kufanya hivyo ili kuepusha malimbikizo ya madai yasiyokuwa ya msingi na kujiingiza katika migogoro isiyo ya lazima baina ya Manispaa na walimu.

Aliongeza kuwa kutokana na mgomo huo kutohusiana na madai ya madeni ya nyuma suala la mgomo huo wa walimu unashughulikiwa katika ngazi nyingine zinazohusika kwa kuwa ni mgomo wa Kitaifa.

Aidha kaimu Mkurugenzi huyo wa Manispaa ya Musoma amewataka Madiwani kuwashirikisha Wananchi katika kufanya maandalizi ya kukamilisha baadhi ya maboma ya madarasa kwa ajili ya wanafunzi watakaoingia kidato cha kwanza hapo mwakani.

Aidha katika kikao hicho cha Baraza la Madiwani kimemchagua diwani wa kata ya Mwisenge (CHADEMA) Bwire Nyamwero kuwa naibu Meya wa Halimashauri ya Manispaa ya Musoma kuchukua nafasi ya mtangulizi wake diwani wa kata ya Kamnyonge Angera Lima.

Katika hatua nyingine Katibu wa Chama Cha Walimu Mkoani Mara (CWT) Fatuma bakari alisema sula la mgomo ambao wameuanza jana utaendelea kuwepo hadi pale watakapo pata maelekezo mengine kutoka kwa viongozi wao wa Kitaifa.

BINDA NEWS liliwashuhudia wanafunzi katika Manispaaya musoma wakicheza nje ya nadarasa huku wengine wakionekana wakizunguka mitaani kutokanana kile kinachoonekana walimu kuendelea kuwa katika mgomo.

No comments:

Post a Comment