MASHINDANO YA NGOMA ZA ASILI YA BALIMI EXTRA LAGER 2012 KUTIMUA VUMBI KUANZIA JUNI 30.
Dar Es
Salaam, June 25th 2012:
Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), kupitia bia yake ya Balimi
Extra Lager, leo imezindua rasmi mashindano ya ngoma za asili ya Balimi Extra
Lager kwa mwaka 2012. Mashindano haya ambayo yametokea kupendwa sana na wakazi
wa kanda ya ziwa yanatarajiwa kuanza kutimua vumbi katika mikoa mbali mbali ya
kanda ya ziwa kuanzia Juni 30.
Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi huo
Jijini Dar es Salaam, meneja wa Bia ya Balimi Extra Lager Bi. Edith Bebwa
alisema; Bia ya Balimi Extra Lager imekuwa ikiendesha mashindano haya maarufu
kama “Mashindano ya Ngoma za Asili ya Balimi Extra Lager” kwa zaidi ya miaka saba sasa , na kwa kweli napenda
kusema kuwa ni mashindano yaliyotokea kupendwa sana katika kanda yetu hii ya
ziwa,
Lengo kuu la kudhamini mashindano haya ni kushirikiana na wakazi
wa kanda ya ziwa katika kuenzi na
kulinda tamaduni za kanda alisema Bi Edith .
Kwa mwaka huu wa 2012, mashindano yataanza rasmi tarehe
30 Juni katika ngazi za mikoa na kumalizika tarehe 21
Julai. Tutaanza na mkoa wa Mwanza ukifuatiwa na mikoa ya Mara, Kagera,
Shinyanga na Tabora, katika mpangilio ufuatao.
Tarehe
|
Mkoa
|
Viwanja
|
30/06/2012
|
KAGERA
|
Kaitaba
|
07/07/2012
|
MWANZA
|
Ccm Kirumba
|
14/07/2012
|
TABORA
|
Chipukizi
|
21/07/2012
|
SHINYANGA
|
Shycom
|
21/07/2012
|
MUSOMA
|
Bwalo la Magereza
|
28/07/2012.
|
FINALS MWANZA
|
Ccm Kirumba
|
Akielezea juu ya zawadi za mwaka huu, bi. Edith Bebwa
alisema; kama ilivyo ada ya Bia ya Balimi, kila mwaka tumekuwa tukiongeza
zawadi ili kuongeza chachu ya ushindani na kuleta tija kwa washindani. Kwa
mwaka huu tumeongeza zawadi kwa takribani asilimia 20 ukilinganisha na mwaka
jana. Hii yote inaonesha jinsi gani bia ya Balimi inatambua, inajali na
kuthamini utamaduni wa kanda yetu. Zawadi kwa washindi ni kama ifuatavyo;
|
Ngazi
ya mkoa
|
Finali
|
Mshindi wa kwanza
|
600,000
|
1,100,000
|
Mshindi wa pili
|
500,000
|
850,000
|
Mshindi wa tatu
|
400,000
|
600,000
|
Mshindi wa nne
|
300,000
|
500,000
|
Mshindi
wa tano hadi wa kumi kila kikundi
|
150,000
|
250,000
|
Pamoja na zawadi hizi nono, pia Balimi
Extra Lager itaendelea kutoa huduma muhimu kwa vikundi shiriki kama vile chakula
na malazi. Tunaamini kabisa mambo yote haya yataongeza hamasa na msisimko
katika mshindano ya mwaka huu. Na kauli mbiu yetu kwa mwaka 2012 “Balimi
Extra Lager, twajivunia utamaduni wetu”.
Akizungumzia maandalizi ya fainali hizo, Meneja Masoko wa
Tbl Fimbo Buttalah alisema; Maandalizi yote kwa upande wetu sisi wadhamini
yameshakamilika, hivyo niwaombe tu washiriki wote ambao nimepata taarifa kuwa
wamekuwa mazoezini kwa muda sasa, waendelee na mazoezi ili kuonesha uwezo wa
juu utakaoleta ushindani na kutoa burudani yenye kiwango cha juu.
Kwa niaba ya bia ya Balimi Extra Lager, tunapenda
kuwakaribisha watu wote kuhudhuria mashindano haya ambayo tarehe na mahali
yatakapofanyikia zitakuwa zikitangazwa redioni ili waweze kushuhudia burudani
hii na kuuenzi utamaduni wetu. Pia wananchi wasisahau kuwa katika burudani hizi
pia wataburudika na Bia yao waipendayo ya Balimi Extra lager baridi, na kushinda
zawadi mbali mbali katika promosheni za Balimi zitakazoambatana na Mashindano
haya ya Ngoma za asili ya Balimi Extra Lager.
Kwa Maelezo zaidi wasiliana na:
Edith
Bebwa, Brand Manager, +255767266410, edith.bebwa@tz.sabmiller.com
Fimbo Butallah, Marketing Manager, +255767266567, fimbo.butallah@tz.sabmiller.com
Editha Mushi, Communications & Media Manager,
+255767266420, editha.mushi@tz.sabmiller.com
Kuhusu TBL
Tanzania
Breweries Limited (TBL) inatengeneza, kuuza na kusambaza bia, vinywaji vyenye
ladha ya matunda vilivyo na kilevi na vinywaji visivyo na kilevi hapa Tanzania.
TBL pia ndiyo kampuni mama ya Tanzania Distilleries Limited pamoja na kampuni
shiriki ya Mountainside Farms Limited.
Bia
zinazotengenezwa na kampuni ya TBL ni pamoja na Safari Lager, Kilimanjaro
Premium Lager, Ndovu Special Malt, Castle Lager, Vinywaji vingine
vinavyotengenezwa na kundi la makampuni ya TBL ni Konyagi Gin, Amarula Cream,
Redd’s Premium Cold na Grand Malt.
Kundi la
makampuni ya TBL limeorodheshwa kwenye Soko la Hisa la Dar es Salaam, limeajiri
watu wapatao 1,300 na linawakilishwa nchi nzima na viwanda vinne vya bia,
kiwanda kimoja cha kutoneshea, kimoja cha kutengenezea kimea pamoja na bohari
nane za kusambazia bia.
Kuhusu SABMiller
SABMiller plc
moja kati ya makampuni makubwa ya bia duniani ikiwa na mikataba ya kutengeneza
na kusambaza bia kwenye nchi zaidi ya 60 katika mabara matano. Bia zake ni pamoja
na zile za kimataifa kama Miller Genuine Draft, Peroni Nastro Azzurro na
Pilsner Urquell vilevile na bia nyingine zinazoongoza kwenye masoko ya ndani ya
nchi mbalimbali. Nje ya Marekani, SABMiller ni moja ya kati ya makampuni
makubwa yanayotengeneza vinywaji vya Coca-Cola duniani. Hivi karibuni SABMiller
plc ilinunua kampuni ya bia ya Foster’s pamoja na shughuli zake za uzalishaji
nchini India.
SABMiller
imeorodheshwa kwenye masoko ya hisa ya London na Johannesbur
No comments:
Post a Comment