SERIKALI imewataka Watanzania kuenzi Utamaduni ambao  utakua kichocheo za kuzuia  maovu ndani ya jamii hasa  katika vita  dhidi ya vitendo vya Rushwa,Unyanyasaji wa Wanawake na  Watoto,Ujambazi,Uporaji na Mauji ya kinyama ambayo yamekuwa yakifanywa  kwa imani potofu.
     Waziri wa habari,vijana utamaduni na michezo Mh Dk  Emanuel Nchimbi,ametoa kauli hiyo mjini musoma wakati  wa kilele cha  maadhimisho ya siku ya utamadini duniani, ambapo kitaifa imefanyika  mjini Musoma mkoani Mara.
     
     Amesema ni imani yake kuwa endapo kila mtu atauenzi  utamaduni wake hakutakuwepo mambo hayo maovu ndani ya jamii hivyo  kuwataka watanzania kutafakari kwa kina maovu hayo kwa kuachana nayo ili  amani na utulivu viimarike na kutawala hapa nchini.
     
     Mh Dk Nchimbi,amesema mila na desturi zikitumika  vizuri ni ukweli zitasisitiza kufanya kazi kwa bidii,kuzalisha  mali,kuheshimu  madaraka na mengine mengi na hivyo kuliwezesha taifa  kusonga mbele kwa kila Nyanja kikiwemo kilimo na kuhakikisha nchi  inakidhi kwa mahitaji yake hasa chakula.
     
     Kw upande wake katibu mkuu wa wizara  ya  habari,vijana,utamaduni na michezo, Bw Sethi Kamuando,akizungumza katika  kilele hicho amesema  hivi  sasa kumeibuka kundi la  baadhi ya viongozi  wa siasa ambao wamekuwa wakitumia mgongo huo kuwagawa wananchi  jambo  ambalo amesema ni dalili mbaya zinazotishia  umoja na  mshakamano  nchini.
     Kilele hicho chenye kauli mbiu TUSHEREKEAPO MIAKA 50  YA UHURU TUDUMISHE UTAMADUNI WETU,zimefanyika katika uwanja wa  kumbukumbu ya Karume na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa serikali  na vyama vya siasa.
No comments:
Post a Comment