Sunday, January 16, 2011

MAPIGANO YA TARIME YANA HISTORIA KUBWA MDAU

 Haya ni maeneo ya mpakani mwa Nchi za Tanzania na Kenya
 Tuliamua kuvuka mpaka tukaingia sehemu ya nchi ya Kenya ili kuona wenzetu wanaishi vipi
 Bado tuko sehemu ya pili ya Mpaka yaani nchini Kenya
 Hatukuwa na gari tuliamu kupaki gari na kuanza kutembea kwa miguu kama ujuavyo kwa kufanya hivyo tuliweza kuona mengi
 Moja ya mambo ambayo tuliyaona ni kama hivi,sio kwetu Tanzania tu ndio watu hawazingatii suala la usafi hata nchi ya Jirani(Kenya) hali ni hiyo hiyo
 Katika hotel hii tulifika japo kupata kinywaji lakini hatukuweza kupata kutokana na sheria ya Kenya kuwa hawaruhusiwi kuuza wakati wa kazi mpaka majira ya saa kumi na moja jioni
 Kesho yake tulianza safari ya kwenda maeneo ambayo huwa kuna mapigano ya Mara kwa Mara mjini Tarime,hii ni shule ya Kubiterere ambapo inasemekana hapo ndipo kuna uwanja wa mapigao wa koo zinazopigana mara kwa mara wilayani humo
  Shule zingine zahitaji moyo kupata elimu bora
 Huyu ni mmoja wa  walimu katika shule hiyo na hapa alikuwa akitupatia historia kuhusu mapigano ya huko na nini kifanyike ili mapigano haya yaishe
             Huu ndio uwanja wa mapigano
                    Uwanja wa mapigano jamani
 Baada ya hapo tuliingia mpaka shule ya sekondari Mwema na kukuitana na walimu wa shule hiyo ambao pia walitueleza kuwa shule hiyo ipo kwenye mpaka ambao wapiganaji hujipanga na kuanza kurushiana mishale
  Maelezo yanaendelea
 Baada ya walimu nilikutana na huyu mzee ambaye ni mwenyeji wa eneo hilo ambapo pia alitueleza kiini cha mapigano
 Mdau  kuna sehemu mawasiliano mpaka utumie mbinu mbadala hili upate mawasiliano
 Baada ya shule ya Mwema tulifika katika kijiji cha Susuni na kukutana na mtanzania huyu ambaye anasema aliwahi kushiriki mara mbili mapigano hayo
 Huyu babu alimpoteza mke wake ambaye aliuawa katika mapigano  ya mwisho
 Pamoja na yote lakini mwanamke kuchunga Ng'ombe katika jamii ya wakurya ni jambo la kawaida sana
  Kazi inaendelea hapa,lakini kipindi namuomba mama huyo nimpige picha ili nitumie kwenye blog yangu alinihisi kuwa natokea jamii ya Walyanchoka na kumpiga picha ni kama vile nataka kuiba ng'ombe hizo ila baada ya maongezi ya takriban dk 3 tulielewana na kukubali kupigwa picha


 
Hali ya Tarime kwa Kilimo ni bomba ile mbaya kwanini watu wasiwekeze kwenye kilimo?
 Baada ya ziara yetu ya mafanikio tuliamua kurudi home,na hapa Sefroza Joseph ambaye alikuwa amenipa shavu kwenye gari yake akiwa amepozi baada ya kuchoka kuendesha
Binti yupo kamini barabarani ila ............................................

Mdau hibvi karibuni nilikuwa wilayani Tarime maeneo ya Sirari ambapo huwa kuna mapigano ya koo mbalimbali za jamii ya wakurya,kuna mengi ambayo waliongea kuhusu mapigano hao.

Taarifa zaidi mdau kuhusu nini walichokiongea nitakuandika baadaye ili uweze kujua kwanini mapigano hayo huwa hayaishi?

No comments:

Post a Comment