Wednesday, December 29, 2010

MIRADI YA TASAF INALIWA NA WAJANJA WACHACHE

Hili ni moja ya jengo ambalo limefadhiliwa na TASAF lakini kwa sasa limeonekana kuchakaa kutokana ni ujenzi kuwa chini ya kiwango
       Meya wa Manispaa ya Musoma Alex Kisurura akitazama sakafu iliyovunjwa na wanakamati wakidai eti ni mbovu baada ya kuletewa fedha zingine za kukamilishia jengo


   Wajumbe waliokuwa katika ziara hiyo wakiangalia ratiba kabla ya kuanza ukaguzi
 Mratibu wa mfuko wa TASAF Bi Grace Muniko akiwa na injinia wa Manispaa katika ziara hiyo
                                         Bi Grace Muniko
       Mmoja wa wenyeviti katika kamati za ujenzi akifafanua jambo kwa viongoiz wa halmashauri
                                                    Injinia akitoa ufafanuzi
                                                   Injinia akitoa ufafanuzi
                                         Injinia akiwa amepozi baada ya ufafnuzi
                           Meya Alex Kisurura akitazama sakafu iliyotolewa wakidai mbovu
                                                             TASF
                          Meya wa Musoma Alex Kisurura na Bi Grace Muniko


                              Tazama jengo la serikali mbao zinazotumika
             Mhe Mbunge wa Musoma mjini Vincent Nyerere akitoa ufafanuzi



            Vijana hawakuwa nyuma katika kuhakikisha kama kweli watu wanawekwa kiti moto

                                                      Ufafanuzi
 Kifaa cha maabara kikiwa chini yaani zahanati haina meza na mh Mbunge aliahidi kuwapelekea meza
                              Mh Mbunge Nyerere akitazama chumba cha uzazi

                                  Wazee hawa walimtafuta mbunge kumpatia hongera ya ushindi
                                      Jamani ndio elimu yetu hakuna sakafu fedha watu wamekula

 Diwani wa Iringo kulia akieleza ujumbe huo kuwa hana taarifa juu ya uakaguzi huo na aligoma kutoa ushirikiano

Miradi inayotolewa na TASF imeonekana kuwanufaisha wachache katika manispaa ya Musoma mkoani Mara baada ya ziara iliyofanywa na mbunge wa jimbo la Musoma Vincent Nyerere na Meya wa manispaa hiyo Alex Kisurura.


Katika ziara hiyo tulishuhudia baadhi ya miradi iliyotolewa na mfuko huo katika awamu ya kwanza ilikuwa imebomolewa huku wenyeviti wa kamti za ujenzi wakijiandaa kurudia eneo hilo tena katika kujenga


Katika hali hiyo Mbunge wa jimbo La Musoma alisema kuwa inashangaza kuona watu wachache ambao wamepewa dhamana ya kusimamia mali ya umma wanafanya mambo ambayo hayafai.


Naye Meya wa Manispaa ya Musoma alisema kuwa katika kipindi hiki cha uongozi wake atajitahidi kila fedha inayotolewa na wafadhili inasimamiwa kama ilivyokusudiwa

Aidha katika ziara hiyo kitu cha kushangaza ni pale ambapo diwani wa kata ya Iringo aligoma kupokea ujumbe huo akidai kuwa hana taarifa

No comments:

Post a Comment