Tuesday, December 21, 2010

MATUMIZI MABAYA YA RASILIMALI ZA UMMA










Mdau siku ya jumapili dreva wa gari la manispaa ya Musoma alikamatwa na uongozi wa manispaa hiyo akifanya kazi za nje badala ya kazi za umma kama kubeba taka na nyinginezo,katika sakata dreva inasemekana alichukua gari na kwenda kubeba taka ili akazitu
pe maeneo ya buhare eneo ambalo limetengwa kwa ajili ya kuwekwa uchafu ingawa hata hivyo si sehemu salama kwa maisha ya binadamu.

Baada ya  kumwaga uchafu alichukua mchanga na kwenda kuumwaga sehemu aliyokuwa amepata tender hiyo lakini kama wasemavyo za mwizi ni 40 wakati anarudia trip nyingine ndipo alipokutana na nguvu ya umma ambao walitoa taarifa kwa viongozi hao na kuja kumkamata,alisindikizwa na gari la polisi moaka kituo kikuu cha polisi nmjni Musoma na hatua zaidi za kisheria na kinidhamu zitachukuliwa dhidi yake.

No comments:

Post a Comment