Wednesday, September 5, 2012


VIONGOZI WA VYAMA VYA WAANDISHI WA HABARI KUTOA TAMKO JUU YA KIFO CHA DAUDI MWANGOSI

Mwenyeviti  na  Makatibu wa vyama vya waandishi wa Habari Mikoa Mbalimbali Tanzania  Wanaanda Utaratibu wa Kutoa tamko juu ya Waandishi waliopo katika Vyama hivyo kutoa tamko kufuatia kifo cha aliyekuwa Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa habari mkoa wa Iringa Daudi Mwangosi.

      Mwenyekiti wa MRPC (MARA) Bw Emmanuel Bwimbo

Akizungumza kwa njia ya simu kutoka jijini Dar es Salaam,Mwenyekiti wa Chama cha Waandishi wa Habari mkoa wa Mara (MRPC) Emmanuel  Bwimbo amesema kuwa katika mkutano utakaofanyika kesho katika hotel ya Lion  viongozi hao wamekusudia kutoa tamko juu ya kifo cha Daudi Mwangosi mikononi mwa Polisi.

Bwimbo amesema kuwa kusudio lao kubwa ni kutoa tamko la wanachama wa Vyama hivyo ambao waandishi wa habari kutofanya kazi pamoja na Jeshi la Polisi hapa nchini kama wahuska katika tukio hilo hawatachukuliwa hatua

Amesema ni unyama mkubwa ambao Jeshi la Polisi wamefanya kwa Mwenyekiti huyo wa Chama cha Waandishi wa habari Mkoa wa Iringa hivyo ni bora nao wakachukua hatua.

   “Hapa mimi nadhani kesho lazima tutoe tamko juu ya hawa waliohusika katika Unyama huu,haiwezekani Mwandishi  Daudi akafa mbele ya Polisi na hao Polisi wakashindwa kuchukuliwa hatua  haiwezekani”?

No comments:

Post a Comment