Monday, August 6, 2012

   WANANCHI TARIME WATAKIWA KUJIKITA KATIKA KILIMO

Dinna Maningo,Tarime

WANANCHI Wilayani Tarime wametakiwa kujikita katika kilimo cha mazao mbalimbali  kutokana na Wilaya hiyo kuwa na misimu miwili ya kilimo na kuwa endapo watawekeza kwenye kilimo itawasaidia kujiendesha  kimaisha wao na familia zao.

Akiongea na ofisini kwake  Ofisa kilimo wa Wilaya ya Tarime Selvanus Gwiboha alisema kuwa Wilaya ya Tarime ina uhakika wa chakula kwa mwaka  na ardhi yenye rutuba ya kutosha ambapo alisema kuwa katika msimu huu wa masika Wilaya inatarajia kuvuna  tani 180,106 nakuwa msimu wa vuli utaanza Septemba 2012 hadi Januari 2013.



“wananchi wawekeze kwenye kilimo wasibweteke,kilimo ni uti wa mgongo watu wasiache kulima mazao yanafaida kubwa unauza na unayatumia  kwa chakula na mahitaji mengine,mazao yanayolimwa Tarime ni mihogo,mahindi,mtama,ulezi,mpunga,viazi vitamu,viazi mviringo na maharage na kwa upande wa mazao ya biashara ni kahawa na ndizi na mikakati inawekwa kulima alizeti na ufuta”alisema Gwiboha.

Gwiboha alisema kuwa kwa Wilayani hapa eneo linalofaa kwa kilimo ni Hekta 790,630 ambapo eneo linalolimwa ni Hekta 69,155 sawa na asilimia 76.30 eneo linalofaa kwa kilimo.

Alisema kuwa eneo linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji ni Hekta 8,643 na linalolimwa ni Hekta 6 sawa na asilimia 0.07 nakwamba zana zilizopo ni matrecta 12 ndiyo pekee hutumika kwa shughuli za kilimo huku plau zilizopo ni 9,495.

Gwiiboha aliongeza kuwa kwa upande wa upokeaji na usambazaji wa vocha za pembe jeo Wilayani Tarime ilipokea jumla ya Vocha 18,000 za kutosheleza wakulima 18,000 sawa na ekari 18,000,mbolea tani 18,000,Urea tani 18,000 na mahindi chotara tani 18,000 nakwamba thamani ya vocha zote ni 1,296,000,000, pia jumla ya vijiji 89 vimenufaika na ruzuku za pembe jeo.

No comments:

Post a Comment