Baadhi ya Wananchi
katika wilaya ya Butiama mkoani Mara wametoa ya moyoni kwa kumuomba aliyekuwa
waziri wa nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo kugombea nafasi ya urais
wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi CCM .
Wakiongea
kwa nyakati tofauti katika kijiji cha Kiriba kata ya Bwai halmashauri ya Musoma
Vijiji,wananchi hao walisema kuwa wamefika hatua hiyo ya kumuomba Profesa
Muhongo baada ya kuridhishwa na utendaji wake wa kazi wakati akiwa katika
wizara ya nishati na Madini na hasa kwa kitendo chake cha kuwakumbuka watu wanaoishi vijijini.
“Mwaka huu
lazima nipige kura kwa Chama cha CCM pale watakapomsimamisha Prof Muhongo kuwa
mgombea wa chama hicho,sikuwahi kufiria katika miaka niliyobakiza hapa duniani
ningeuona umeme maana toka uhuru huku hata nguzo hatukuziona ila muhongo
kafanya jambo la kishujaa sana”alisema Bw Joseph Magoti mkazi wa Bwai
Kwitululu.
Mbali na
Bwana Joseph kuelezea kile ambacho alisema kina msukumu kumshaiwishi Prof
Muhongo kugombea nafasi hiyo lakini pia baadhi ya akina mama walipata nafasi ya
kutoa maoni yao kuhusu hatua hiyo walidai kuwa kupelekwa kwa umeme katika
vijiji mbalimbali hapa nchini imesaidia kupunguza umaskini kwa wananchi walio
wengi.
Bi Sophia
Matiku aliyesema kwasasa amebadili maisha yake kufuatia kuwepo kwa nishati ya
umeme katika kijiji hicho alisema haoni sababu ya Prof Muhongo kutogombea
nafasi hiyo kwani wale wote waliotajwa katika kinyang’anyiro hicho bado
wanapwaya kutokana na utendaji wao katika nafasi walizoweza kushika.
“Wanasema
mnyonge mnyongeni haki yake mpeni,huyu Profesa kiukweli kwa muda mfupi aliokaa
kwenye ile wizara ya umeme (Nishati na Madini) alifanya kazi kubwa sana na kama
angekuwepo tangu Rais Kikwete anaingia madarakani leo vijiji vyote vingewaka
umeme,kwa kweli katika hilo mimi naomba agombee nafasi ya urais ili na sisi
wanyonge tusaidiwe”alisema Bi Sophia Matiku.
Hata hivyo
mbali na wananchi hao kuta sifa hizo kwa aliyekuwa waziri wa nishati na Madini
Profesa Sospeter Muhongo,Bw Juma Wambura alisema muda umefika kwa watanzania
kuamua kwa pamoja kumchagua kiongozi ambaye atafanya maamuzi ambayo
yatanufaisha watanzania wote ni kikundi cha watu.
Alisema
msimamo aliounyesha Profesa Muhongo wakati akiwa katika nafasi ya uwaziri wa
nishati na Madini ni mfano tosha kwa kiongozi ambaye anastahili kuiongoza
Tanzania kwasasa.
‘Nchi yetu
leo ina tatizo la viongozi kuwa na maamuzi ambayo atayatoa na kuyasimamia bila
kuogopa mtu lakini kiukweli Profesa anastahili kuwa Rais maana msimamo aliokuwa
nao ndiyo unatakiwa leo hapa nchini.alisema Bw Juma Wambura.
Pamoja na
kuwepo kwa kauli mbalimbali juu ya kumshawishi Profesa Muhongo kugombea nafasi
ya Urais ndani ya Chama cha Mapinduzi,Bw Musa Hassan mkazi wa Mgango ambaye
amewahi kuwa mtumishi katika serikali ya awamu ya pili alisema kuwa angependa
Profesa Muhongo kuwa rais wa awamu ya Tano wa Tanzania ili kusaidia uchumi wa
Tanzania ukue tofauti na sasa.
Alisema
pamoja na kuamini Profesa Muhongo anaweza kukuza uchumi wa Tanzania zaidi ya
hapa lakini pia ukusanyaji wa kodi utaongezea mara dufu kwani kwasasa
ukusanyaji wa kodi si mzuri kutokana na mifumo iliyopo ya kukusanya kodi kwa Maskini na kuwaacha
matajiri.
“Kiukweli bado sijaona mtu ambaye anaweza
kuitoa Tanzania hapa ilipo kwani hao wote wanajitangaza hawana uwezo wa kukuza
uchumi wa Tanzania na wakasimamia vyema ukusanyaji wa kodi,nampenda Profesa
sababu hana urafiki na matajiri sasa ukiona mtu wa hivyo hataona haya kumwambia
mtu alipe kodi´alisema Bw Musa Hassan
Kwa nyakati
tofauti baadhi ya makundi mbalimbali yamekuwa yakijitokeza na kumuomba
aliyekuwa Waziri wa nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo kuingia kwenye
kinyang’anyiro cha kugombea nafasi ya urais katika chama cha Mapinduzi lakini
mpaka sasa Profesa Muhongo hajasema chochote.
No comments:
Post a Comment