Kuna lori lililokuwa limebeba kontena limejaribu kupita daraja
linalounganisha UKONGA {BANANA)- SEGEREA- KINYEREZI NA MBEZI
limeharibika kabisa kwa kutumbukia na lori , kwa sasa foleni ni kubwa
magari yote yanarudi, kwa wanaotoka mjini ni vyema kutumia njia ya
VINGUNGUTI kwenda KINYEREZI, SEGEREA NA MBEZI,
Daraja limearibika sana.
NI VYEMA SHERIA IKACHUKUA MKONDO WAKE, haiingi akili mjinga mmoja kukata mawasilino wa watu wote kwenye njia muhimu kama hii.
Mfumo wa kudhibiti malori ya mizigo ni dhaifu sana nchini, madereva
wangepewa route za kupita pale wanapotoa mizigo bandari na wanapoingiza
mizigo hapa mjini kutoka mikoani,
Bila shaka jamaa wametumia mwanya wa polisi/trafic kutofanya kazi usiku
kufanya huu utumbo, hivi kwa nini usiku kwa mji mkubwa kama Dar jeshi la
polisi linalala mapema HIVYO?
No comments:
Post a Comment