Serikali
wilaya ya Bunda Mkoani Mara imesitisha Mashindano ya Esther Bulaya ambayo
yamekuwa yakifanyika kila Mwaka wilayani humo kwa kile kinachodaiwa baraza la
michezo wilayani humo kutoridhishwa na Mazingira ya uwanja wa Sabasaba
unatumika kwa Mashindano hayo.
Mwenyekiti
wa Mashindano hayo ya Esther Bulaya Bw Flavian Nyamageko alisema Mashindano
hayo yamekuwa yakifanyika katika uwanja huo lakini pia wakishirikisha viongozi
wa chama cha Soka wilayani humo lakini leo wanashangazwa na kitendo cha chama
hicho cha soka kusitisha Mashindano hayo
Mwenyekiti
huyo alisema kuwa alipojaribu kuuliza sababu ya kusitishwa kwa Mashindano
hayo viongozi wa Chama cha Soka wilaya
ya Bunda wamemweleza ni agizo kutoka kwa mkuu wa wilaya.
'Tumekuwa tukifanya haya Mashindano kila mwaka
tena kwa ufanisi Mkubwa,juzu tumeanza mashindano baada ya kupewa kibali na
Chama cha Soka wilaya lakini tunashangaa leo tunaambia tusifanye Mashindano
hayo kwa sababu ambazo hazina msingi"alisema Mwenyekiti huyo
Akieleza
sababu ambazo zimeainishwa katika barua hiyo Bw Nyamagelo alisema kuwa zipo
sababu tatu ambazo zimeelezwa kuwa ni Mazingira kutokuwa rafiki ya
kiuchezaji,Chombo kinachotakiwa kuendesha mashindano hayo ni Chama cha Soka na
si mwingine,kutokuwepo kwa usalama wa kutosha kulingana na watu wanaohudhuria.
Kiukweli
kwetu sisi tunaona hii ni kupingana na ilani ya chama cha Mapinduzi katika
kuendeleza Michezo,aliongeza kuwa huu ni mwaka wa nne katika kuandaa mashindano
hayo.
Alipotafutwa Afisa Michezo wilaya ya Bunda mkoani hapa Bw
Amos Mtani alisema ofisi yake bado haijapokea
barua yoyote inayoonyesha kusitishwa kwa Mashindano hayo ingawa nakala ya barua
hiyo ambayo waandishi wa habari wameipata wilayani hapa inaonyesha kueleza kutekeleza agizo la Mkuu wa wilaya
hiyo lakini afisa michezo huyo hakufika katika kikao hicho.
Wakiongea
kwa jazba na waandishi wa habari baadhi ya wadau wa soka wilayani hapa walisema
kuwa ni hatari sana kama suala la kisiasa linaingia katika michezo maana kwa
hilo inaonekana ni mambo ya kisiasa.
Bw
Marwa Juma ambaye alisema kuwa amekuwa mfuatiliaji wa mashindano hayo tangu
yameanza amesikitishwa na kusitishwa kwa Mashindano hayo ya Esther Bulaya Mwaka 2014 kwa kile kinachodai hali ya
kiusalama si nzuri lini fujo ilitokea ? alihoji bw Juma
"Tukiendelea
kuchanganya chuki na siasa hatutainua michezo katika wilaya yetu" alisema
Bw Marwa
Akiongea kwa njia simu kutoka Dar es Salaam Mbunge wa Viti Maalum Vijana Mkoani Esther Bulaya alisema bado anaendelea kuwasiliana na waratibu wa Michuano hiyo lakini hakuna mtu wa kuweza kuizua kwani hiyo ni sera ya Chama cha Mapinduzi.
"Na mimi nimesikia suala hilo na bado naendelea kuwasiliana na waratibu ingawa sidhani kama kuna mtu anaweza kuzia Mashindano hayo kwani hiyo ni sera ya Chama cha Mapinduzi"Alisema Bulaya
Akiongea kwa njia simu kutoka Dar es Salaam Mbunge wa Viti Maalum Vijana Mkoani Esther Bulaya alisema bado anaendelea kuwasiliana na waratibu wa Michuano hiyo lakini hakuna mtu wa kuweza kuizua kwani hiyo ni sera ya Chama cha Mapinduzi.
"Na mimi nimesikia suala hilo na bado naendelea kuwasiliana na waratibu ingawa sidhani kama kuna mtu anaweza kuzia Mashindano hayo kwani hiyo ni sera ya Chama cha Mapinduzi"Alisema Bulaya
Mashindano ya Esther Bulaya
yamekuwa yakifanyika kila mwaka kwa misimu minne Mfululizo kwa kuandaliwa na
Mbunge wa viti Maalum kupitia vijana ambapo yamekuwa yakiibua vijana mbalimbali ambapo mwaka huu yanashirikisha
timu 72 na wachezaji 1440 katika vituo
vya Bunda,Mgeta na kituo cha Nyamswa
No comments:
Post a Comment