Monday, March 31, 2014

Wadau wa Soka Mara walalamikia Chama Soka Mara (FAM)

WADAU wa soka mkoani Mara wamekitupia lawama chama cha soka mkoani humo(FAM) kwa kile walichodai kuitengenezea mazingira timu ya JKT Rwamkoma kuchukua ubingwa ili iuwakilishe mkoa.

Wakizungumza mara baada ya mchezo ulioipa ushindi wa mabao 12-0 JKT dhidi ya timu ya Wasaga FC,wadau na mashabiki wa soka walidai tangu mwanzoni mwa ligi(FAM)wamekuwa wakiitengenezea mazingira timu hiyo kwa kile walichokidai kuziona timu nyingine haziwezi kusafiri.

Walisema katika mchezo huo JKT Rwamkoma walikuwa hawana uwezo wa kutoka na matokeo hayo ya ushindi kutokana na mchezo huo na kuiomba TFF kufatilia kwa makini na kuomba taarifa ya mchezo kutokana na mazingira hayo kuzikatisha tamaa timu nyingine kushiriki ligi msimu ujao.

Mmoja wa dau hao aliyefahamika kwa jina la Philipo Janja alisema kamwe soka la mkoa wa Mara halitaendelea kutokana na kile alichokieleza viongozi kuzikumbatia timu ambazo hazina uwezo na kila msimu mkoa wa Mara wamekuwa wasindikizaji kwenye ligi ya Taifa.

Akitolea mfano timu ya Baruti FC iliyomaliza katika nafasi ya pili kwa kuzidiwa na JKT Rwamkoma kutokana na tofauti ya magori ya kufunga,Janja alisema ilikuwa ni timu yenye wachezaji waliokaa pamoja kuanzia msimu uliopita na hali ya ushindi wa mabao 12 wa JKT Rwamkoma aliodai wa kupangwa umewakatisha tamaa.




"Mimi naweza kusema Baruti Fc ilikuwa ni timu bora kwenye haya Mashindano maana hata ukiangalia mechi zao wanacheza kwa malengo,kwa stahili hii itakuwa ngumu"alisema Janja

Alisema lazima chama cha soka mkoa wa Mara(FAM) ni lazima wabadilike nakuona kila timu inayoingia kwenye mashindano inao uwezo wa kusafiri na kuacha kuzibeba timu ambazo wanadhani zinauwezo na matokeo yake zinakuwa wasindikizaji kwenye ligi ya taifa.

Alipotafutwa ili kuweza kuzungumzia malalamiko hayo ya wadau na mashabiki wa soka mkoani Mara,katibu wa (FAM) Mugisha Galibona hakuweza kupatikana uwanjani wala simu yake ya mkononi huku ikidaiwa alikwenda kutuma jina la bingwa wa mkoa TFF kutokana na kuogopa kuchelewa kulituma.


Katika mchezo wa mwisho timu ya Baruti Fc iliibamiza timu ya Musoma Shooting mabao 3-1 huku timu ya JKT Rwamkoma ikiibuka kidedea kwa kuwa bingwa wa mkoa wa Mara 2014 baada ya kuifunga timu ya Wasaga FC mabao 12-0

No comments:

Post a Comment