Friday, February 14, 2014

PSPF Kunufaisha Watanzania wasiokuwa watumishi wa Umma

Mkurugenzi Mkuu wa PSPF Bw Adam Maingu  akiongea na Mkuu wa Mkoa wa Mara Bw John G.Tuppa

  Mkurugenzi Mkuu wa PSPF akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Mara Kalenda ya Mwaka 2014 Mkuu wa Mkoa wa Mara Bw John G.Tuppa.
  Mkurugenzi Mkuu wa PSPF akizungumza na Wakurugenzi wa Halmashauri na Manispaa Mkoani Mara katika ukumbi wa uwekezaji Mkoani Mara.
  Maafisa wa PSPF
Mjasiriamali Amani Richard akinena jambo
Mkuu wa Mkoa wa Mara Bw John G. Tuppa akinena Jambo katika chakula cha jioni
Nipe paja hilo
MUSOMA
 
MFUKO  wa Pensheni kwa Watumishi wa Umma  PSPF  umetangaza mkakati wa kuwanufaisha Watanzania ambao si watumishi wa umma kwa kujiunga na mfuko  wa uchangiaji kwa hiari wa PSS  huku makundi ya Wajasiliamali,Wavuvi,Wakulima na makundi mengine katika jamii ambayo yamejiajiri katika sekta isiyo rasmi yakipewa kipaumbele katika mfuko huo.
 
Mkurugenzi mkuu wa mfuko wa PSPF Bw Adam Maingu,alitoa kauli hiyo mjini Musoma wakati akizungumza na viongozi,wawakilishi na wanachama wa mfuko huo katika wilaya ya Musoma na Butiama mkoani Mara.
 
Alisema kwasasa mfuko huo wa kuchangia kwa hiari utakuwa ni mkombozi mkubwa kwa makundi mbalimbali yakiwemo ya watumishi wa Umma,Sekta binafsi na wafanyabiashara kujiwekea akiba kwa kuchangia kiasi cha kuanzia elfu kumi na kuendelea.
 
Kwa upande wake mkuu mkuu wa mkoa wa Mara Bw John Gabriel Tuppa,akizungumza katika hafla hiyo,ameupongeza uongozi wa mfuko huo kwa kukutana na wadau wake kwaajili ya kupata maoni ambayo yatasaidia kuboresha utendaji wao wa kazi
lakini akiwataka watendaji wa Mfumo huo kujenga imani kwa wanachama wao endapo watapunguza gharaza za uendeshaji ili gharama zingine zirudi kwa wanachama
 
Nao baadhi ya washiriki katika hafla ambayo ni watumishi wa Serikali na Sekta binafsi wametoa maoni mbalimbali katika kuboresha Mfuko huo huku wakitaka wanachama kupewa kadi za uanachama

No comments:

Post a Comment