MAKAMU wa Rais Dkt Mohamed Gharib Bilal amesema kuwa Serikali ya awamu 
ya nne itaendeela kujenga mazingira mazuri ya uwekezaji hapa nchini kwa 
lengo la kuvutia wawekezaji wa ndani na nje ya nchi.
Makamu Rais Dkt Bilal ameyasema hayo jijini Mwanza wakati akifungua 
kongamano la siku tatu la uwekezaji lililoandaliwa na Mikoa sita ya 
Kanda ya Ziwa katika Hoteli ya Malaika Beach Resort na kuwashilikisha 
washiriki zaidi ya 1000 toka ndani na nje ya nchi.
Alisema kuwa Serikali tayari imechukua hatua za makusudi kuboresha 
mazingira ya Uwekezaji katika kuanzisha na kufungua biashara,kupunguza 
urasimu wa upatikanaji wa leseni za biashara,uboreshaji wa sheria za 
mikataba ya kazi.
“Kwa kiwango kikubwa Serikali imedhibiti rushwa na kurekebisha masuala 
ya ksiera na sheria lengo likiwa ni kuhakikisha inavutia wawekezaji hapa
 nchini”,alisema Makamu wa Rais Dkt Bilal
.
.
Dkt Bilal alisema kuwa ili kuwe na uhakika wa masoko kwa bidhaa 
zinazozalishwa na wawekezaji wa ndani,Serikali imeingia mikataba 
mbalimbali na maridhiano katika uwekezaji na amsoko ya kimataifa kwa 
kushirikiana na AGOA,SADC,na COMESA. 
Makamu wa Rais aliipongeza Mikoa ya Kanda ya ziwa kutokana na kuamua 
kufanya Kongamano hilo muhimu kwa ajili ya kutangaza vivutio vya utalii 
pamoja na raslimali zilizopo katika Mikoa ya kanda ya ziwa.
Alisema kuwa mikoa hiyo imebahatika kuwa na idadi kubwa ya watu pamoja 
na raslimali lukuki ambazo zinahitajika kuendelezwa kwa ajili ya 
kuongeza pato la taifa.
Source Gsengo
Source Gsengo
 Mkuu
 wa Mkoa wa Mwanza Everist Ndikilo alisema kuwa wakuu wa mikoa wa Mikoa 
ya Kanda ya ziwa waliafikiana kufanya kongamano la kuvutia wawekezaji na
 kueleza kuwa kongamano hilo ni la aina yake kufanyika hapa nchini kwa 
kuandaliwa na mikoa sita kwa pamoja.
Mkuu
 wa Mkoa wa Mwanza Everist Ndikilo alisema kuwa wakuu wa mikoa wa Mikoa 
ya Kanda ya ziwa waliafikiana kufanya kongamano la kuvutia wawekezaji na
 kueleza kuwa kongamano hilo ni la aina yake kufanyika hapa nchini kwa 
kuandaliwa na mikoa sita kwa pamoja.Awali Mwenyekiti wa Kongamano hilo Waziri wa zamani katika Wizara mbalimbali Sir George Kahama,aliitaka Serikali kuhakikisha inakamilisha ujenzi wa uwanja wa ndege wa Mwanza kwa ajili ya kuunganisha mikoa ya kanda ya ziwa na wawekezaji toka ndani na nje ya nchi.
Sir Kahama alisema kuwa uwanja wa ndege wa Mwanza unapashwa kujengwa kwa
 kiwango cha kimataifa na kushangazwa na kusua sua kwa ujenzi wake hivyo
 kuinyima fursa mikoa ya kanda ya ziw akufanya baishara za kimataifa 
kupitia uwanaj wa ndege wa Mwanza.
 
















 
No comments:
Post a Comment