
Rais Kikwete ametangaza siku tatu za kuomboleza kifo cha Mandela,Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete,
ametangaza siku tatu za maombolezi, kufuatia kifo cha mzee Nelsomn
Mandela, akisema kua Afrika na dunia nzima kwa ujumla imempoteza shujaa
mkubwa sana katika karne ya 20 na 21.
Naye Rais wa Rwanda Paul Kagame,amesema kua Mandela ataendelea kuishi kwenye mioyo ya wengi wetu.
Naye Rais mstaafu Daniel Moi ambaye alikuwa madarakani wakati Mandela alichaguliwa kuwa rais wa kwanza mweusi wa Afrika Kusini, amempongeza Mandela kwa kuhakikisha utulivu wa kisiasa barani Afrika na kuwa mfano bora kwa viongozi wengine.
No comments:
Post a Comment