Thursday, October 31, 2013

SIMBA YATOKA SARE NA KAGERA SUGAR, UWANJA WA TAIFA DSM


 Askari wa kutuliza ghasia, FFU, wakipiga mabomu ya machozi hewani kuwatawanya mashabiki wa Simba, waliokuwa wakifanya fujo kwa kung'oa viti na kurusha uwanjani baada ya timu ya Kagera Sugar, kusawazisha bao lao kwa mkwaju wa penati katika dakika ya 90+, iliyotolewa na mwamuzi, Mohamed Theophile. Penati hiyo imepatikana baada ya beki wa Simba Joseph Owini, kumchezea vibaya Daud Jumanne, penati hiyo iliyopigwa na Salum Kanon, imezifanya timu hizo kutoka sare ya 1-1, wakati bao la SImba likifungwa na Amis Tambwe katika dakika ya 45.
 Askari wakimdhibiti mmoja wa mashabiki wa Simba.
****************************************
BAO la beki wa kulia wa Kagera Sugar, Salum Kanoni lilipoteza amani ndani ya Uwanja wa Taifa baada ya mashabiki wa Simba kuanza kung’oa viti hali iliyosababiosha Polisi walipue mabomu ya machozi kutuliza vurugu hizo.
Kagera ambao walikuwa nyuma kwa bao 1-0 lililofungwa na Amisi Tambwe katika kipindi cha kwanza, walipata bao la kusaweazisha kupitia kwa Kanoni kwa njia ya panalti baada ya Joseph Owino kumwangusha Daudi Jumanne katika eneo la hatari.
Kwa sare hiyo hali ya Simba imeendelea kuwa tyete kwani bado wamebaki katika nafasi ya nne wakiwa na pointi 21 nyuma ya Yanga yenye pointi 22 huku Azam na Mbeya City wakiwa juu kwa pointi 23 kila moja wakitofautiana mabao ya kufunga.
Katika mchezo huo ambao ulikuwa na ushindani mkubwa katika dakika zote kwani timu hizo zilikuwa zikihitaji pointi tatu ili wajiweke sehemu nzuri kabla ya kumaliza mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Simba itamalizia mzunguko wa kwanza kwa kucheza na Ashanti United mchezo utakaochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Jumamosi ya Novemba 2. 
 Kipa wa akiba wa Simba, Abel Dhaila, akimlalamikia mwamuzi wa akiba baada ya mwamuzi wa kati kutoa penati katika dakika za majeruhi.

  Kipa wa akiba wa Simba, Abel Dhaila, na Kocha Mkuu, Abdallah Kibaden, wakimlalamikia mwamuzi wa akiba baada ya mwamuzi wa kati kutoa penati katika dakika za majeruhi.
 Wachezaji wa akiba wa Simba wakisikitika baada ya kuamuliwa kupigwa penati hiyo.
 Askari wakiendelea kumdhibiti shabiki aliyekamatwa baada ya mashabiki hao kuvunja viti na kuanza kuruka uwanjani.
Askari wakiendelea kudhibiti vurugu..
 Sehemu ya viti vilivyoharibiwa....
 Wachezaji wa Simba, wakimpongeza beki wao Salum Kanon, baada ya kusawazisha bao hilo kwa mkwaju wa penati.
 Patashika langoni mwa Kagera Sugar.
 Kiungo wa Kagera Sugar, George Kavila (kulia) akimtoka mshambuliaji wa SImba, Amis Tambwe, wakati wa mchezo huo.
 Amis Tambwe, akidhibitiwa.
 Ramadhan Singano wa Simba (kushoto) akijaribu kumtoka beki wa Kagera Sugar, Malegesi Mwangwa.
 Hatari langoni mwa kagera.
 Tambwe akidhibitiwa.

No comments:

Post a Comment