Monday, October 21, 2013

SERENGETI YAJENGA HOSPITAL YA KISASA



Mwenyekiti wa halmshauri ya wilaya ya Serengeti Bw John Ng’oina akiongea na blog hii ametoa Pongezi hizo kwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt Jakaya Mrisho Kikwete wakati akiileza Channel ten hali ya ujenzi wa hospital hiyo.
  
Amesema hospital hiyo ambayo itakuwa ya ghorofa sita na vifaa vya kisasa itakuwa na Msaada mkubwa katika wilaya hiyo ambapo kwasasa wapo kwenye mchakato wa kutafuta fedha ili kukamilisha ujenzi huo.


Mbali na Mradi wa ujenzi wa Hospital hiyo lakini pia ujenzi wa kiwanja cha Ndege na Chuo kikuu kitivo cha Mali asili na utalii imeelezwa itasaidia kuinua hamasa ya elimu katika halamashauri hiyokama wanavyoeleza baadhi ya Madiwani wa halmashauri hiyo.

Ujenzi wa hospital hiyo ya wilaya unafanyika  umbali wa  kilomita 3 kutoka Makao Makuu ya wilaya hiyo katika eneo la Kibeyo ambapo umeanza Mwaka 2008/ 2009 huku ikikadiriwa kugharimu kiasi cha shilingi bilion 13 huku tayari awamu ya kwanza ya ujenzi wa jengo la OPD umefanyika ikiwa pamoja na kulipa fidia kwa Wananchi waliokuwa karibu na eneo la Mradi

No comments:

Post a Comment