MARA
Jeshi la
Polisi Mkoani Mara Linawashikili Watu wawili katika matukio mawili tofauti ya mauaji yaliyotokea katika wilaya za Butiama na Serengeti mkoani humo
jeshi la
Polisi Mkoani humo linamshikilia Balozi kutoka kata ya Etaro Alex Nyarukamo mwenye
umri wa miaka 61 baada ya Kukutwa nyumbani kwake kwa Pikipiki ya Marehemu Magere
Mugeta yenye namba za usajili T.509 BCE.
Kamanda wa
jeshi la Polisi mkoani Mara,Kamishina msaidizi
Mwandamizi Abslom Mwakyoma amesema kabla ya kuuwawa kwa Mwendesha
pikipiki huyo alimgonga mtembea kwa miguu aliyefahamika kwa jina la Majani
katika kijiji cha Nyegina na kukimbia akidhani ameua
Katika tukio
linguine Kamanda Mwakyoma amesema mtu mmoja ameuawa katika kata ya Machochwe
wilaya ya Serengeti mkoani Mara kwa kile kinachodaiwa ni wivu wa Mapenzi ambapo mtuhumiwa wa Tukio hilo Mwita Wambura
amejisalimisha Polisi.
Kamanda
amesema Upelelezi juu ya Matukio hayo umeanza kufanyika ili kubaini na
kuwabaini wahuska wa matukio hayo na
kuwachukulia hatua za kisheria huku
akitoa wito kwa Madereva wa Pikipiki watii sheria bila kushurutishwa na
waepukekujichukulia sheria.
No comments:
Post a Comment