Wednesday, December 5, 2012

UZINDUZI RASMI WA UHURU MARATHON

 
Mbio mpya za Nyika za Uhuru 'Uhuru Marathon' zimezinduliwa hii leo jijini Dar es Salaam naWaziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Dk. Fenela Mukangara. Pichani ni Waziri akiangalia nembo ya Mashindano hayo mapya yatakayo kuwa yakifanyika Desemba 8, ya kila mwaka kuuenzi uhuru wa Tanzania. Pamoja nae ni Mkurugenzi wa Intelecture Communication Ltd, Waandaaji wa Mbio hizo, Innocent Meleck.



Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Dk. Fenela Mukangara akizindua rasmi tovuti ya Mbio hizo ya http://www.uhurumarathon.com pamoja nae ni Mkurugenzi wa Intelecture Communication Ltd, Waandaaji wa Mbio hizo, Innocent Meleck.
 Waziri wa Habari, Utamaduni, Vijana na Michezo, Dk. Fenela Mukangara akizungumza.
 Mkurugenzi wa Intelecture Communication Ltd, Waandaaji wa Mbio hizo, Innocent Meleck akitoa maele
zo juu ya Mashindano hayo.
Meleck akijadiliana jambo na Mgeni Rasmi Waziri wa Habari, Utamaduni Vijana na Michezo.
Meza kuu ikifuatilia matukio mbalimbali.
Wadau mbalimbali wa Michezo na waandishi wa habari walihudhuria.
Mrisho Mpoto 'Mjomba' akighani mashairi yake kama kawaida.
Waikmbaji wa Bendi ya Mjomba, Josephina Johnswam, Ismail Kipira na Twaha Farahani wakiwajibika wakati wa Uzinduzi huo.
Mpoto alishambulia vilivyo na kuisimamisha meza kuu na kuipa maneno mazito juu ya kuuenzi Uhuru wa Tanzania ambao unatimiza miaka 51.

No comments:

Post a Comment