TIMU ya Taifa ya Uganda, The Cranes imefanikiwa
kutwaa Ubingwa wa Mashindano ya CECAFA Tusker Chalenji baada ya kuichapa
timu ya Taifa ya Kenya, Harambee Stars mabao 2-1.
Matumaini ya Kenya kutwaa kombe hilo yalizimishwa tena na Uganda
baada ya kujipatia bao dakika chache kabla ya mpira kumalizika. Uganda
sasa wanaendelea kuwa vinara wa kombe hilo baada ya kulitwaa mara ya 13
wakiwa wanaongoza.
Timu ya mpira wa miguu ya Zanzibar Heroes kutoka mjini Zanzibar
yenyewe imefanikiwa kutwaa nafasi ya tatu katika mashindano ya CECAFA
Tusker Chalenji baada ya kuifunga Kilimanjaro Stars mabao 6-5. Zanzibar
imeifunga Kili Stars ya Tanzania bara baada ya kupigiana mikwaju ya
penati baada ya kumalizika dakika 90 huku timu zote zikiwa sare ya 1-1.
Ndipo mpambano huo ukaariwa zipigwe penati kumpata mshindi wa nafasi ya
tatu.
No comments:
Post a Comment