Rais
wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania na Amiri Jeshi mkuu Dk.Jakaya
Kikwete akiwasili katika gari maalum la Kijeshi na Mkuu wa majeshi
Jenerali Davis Mwamunyange kwenye uwanja wa uhuru kwa ajili ya
maadhimisho ya miaka 51 Uhuru wa Tanzania yanayofanyika kila mwaka
Desemba 9, Kauli Mbiu ya Maadhimisho ya Mwaka huu ni “Uwajibikaji,
Uadilifu na Uzalendo ni nguzo ya Maendeleo ya Taifa letu”
Amiri
Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya muungano ya Tanzania Dk. Jakaya
Kikwete akikagua gwaride la vikosi vya Ulinzi na usalaama katika
maadhimisho hayo.
Amiri
Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya muungano ya Tanzania Dk. Jakaya
Kikwete akikagua gwaride la vikosi vya Ulinzi na usalaama katika
maadhimisho hayo
Kikosi cha Brass Band cha majeshi ya Ulinzi na usalama kikitumbuiza katika maadhimisho hayo
Viongozi mbalimbali wakiwa katika
maadhimisha hayo kutoka kulia ni Rais Joseph Kabila wa Jamhuri ya
Kidemokrasia ya Congo, Mama Maria Nyerere, Rais wa Msumbiji Mh. Armando
Guebuza,Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Dk. Gharib
Bilal na Mzee Ali Hassan Mwinyi rais Mstaafu wa awamu ya pili
Rais
wa Msumbiji Mh. Armando Guebuza akipokewa na Mkuu wa mkoa wa Dar es
salaam Mh Said Meck Sadik mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa Taifa.
Rais
wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Mh. Joseph Kabila akipokewa na
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh Said Meck Sadik mara baada ya kuwasili
kwenye uwanja wa Uhuru asubuhi hii.
Mama Maria Nyerere akiwasili kwenye uwanja wa Uhuru kwa ajili ya kuhudhuria maadhimisho ya miaka 51 ya uhuru wa Tanzania.
Waziri
Mkuu wa Jamhuri ya Muungano ya Tanzania Mh. Mizengo Pinda akiwasili
kwenye uwanja wa Uhuru kuhudhuria maadhimisho hayo huku akisindikizwa na
Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mh. Said Meck Sadik.
Vikosi
vya Ulinzi na Usalama vikiwa vimejipanga tayari kwa gwaride la utii na
heshima mbele ya Amiri jeshi Mkuu na Rais Jamhuri ya muungano ya
Tanzania Dk. Jakaya Kikwete.
Makamu
wa Rais Dk. Gharib Bilal akisalimiana na Mama Fatma Karume mara baada
ya kuwasili uwanjani hapo, katikati ni Waziri Mkuu Mh. Mizengo Pinda.
picha na by John Bukuku
No comments:
Post a Comment