Saturday, December 15, 2012

Askari polisi wanaohudumia kitengo cha dawati la Jinsia Wanawake na Watoto wametakiwa kuwa na kauli nzuri wanapokuwa wanawahudumia wahanga wanaofanyiwa vitendo vya ukatili wanapowafikia.










WANAFUNZI WA TARIME HIGH SCHOOL

WAUMINI WA KANISA LA ANGLICAN NAO HAWAKUWA NYUMA

POLISI WAKIWA KATIKA MAANDAMANO YA MAAZIMISHO YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA WILAYANI TARIME

WATOTO WANAFUNZI WA SHULE NAO WALISHIRIKI

KAIMU KAMANDA ZACHARIA AKIFAFANUA JAMBO


ASKOFU WA KANISA LA ANGLICAN DAYOSISI YA TARIME DK.MWITA AKILI AKISOMA HOTUBA KATIKA UFUNGUZI WA OFISI YA DAWATI LA JINSIA NA MAAZIMISHO YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA

KAIMU KAMANDA WA POLISI KANDA MAALUM YA TARIME RORYA SEBASTIAN ZACHARIA KUSHOTO KATIKA MAAZIMISHO YA SIKU 16 ZA KUPINGA UKATILI WA KIJINSIA NA UZINDUZI WA OFISI YA DAWATI KITUO CHA POLISI WILAYANI TARIME
Na Shomari Binda,Tarime
Askari polisi wanaohudumia kitengo cha dawati la Jinsia Wanawake na Watoto wametakiwa kuwa na kauli nzuri wanapokuwa wanawahudumia wahanga wanaofanyiwa vitendo vya ukatili wanapowafikia.
Kauli hiyo ilitolewa na Askofu wa Kanisa la Anglicana Dayosisi ya 
 Tarime Dk.Mwita Akili alipokuwa akifunga siku 16 za kupinga Ukatili wa Kijnsia sambamba na ufunguzi wa Ofisi ya dawati la Jinsia katika kituo kikuu cha Polisi Wilayani Tarime
Alisema wahanga wa Ukatili hawana budi kuzungumza nao kwa unyenyekevu ili waweze kuelezea kwa umakini yale yaliyowasibu na si vyema kuzungumza nao kwa kuwafokea na kuendelea kuonekana wanyonge.
Askofu Mwita alisema kuanzishwa kwa dawati la Jinsia na ufunguzi  wa Ofisi hiyo kuwe ni chachu ya kuwasaidia Wanawake hasa wale wanaokutana na vitendo vya ukatili pale wanapowafikia kutaka msaada kutoka kwao.
“Watakaowafikia katika ofisi hii ni sawa na mama zenu,dada ama ndugu kwenu hivyo wasaidieni kwa kuzingatia maadili ya kazi na kuwa na moyo wa huruma ili wapate faraja na msifanye kinyume na hivyo.
“Mtu anaye kutana na suala la ukatili anahitaji msaada na kuwa naye kwa ukaribu naamini askari Polisi watakao kuwa katika dawati hili tayari wanayo mafunzo namna ya kuwahudumia wahanga wa Ukatili nawaombea kwa Mungu awape wepesi katikakutekeleza majukumu yenu ya kazi”,alesema askofu Mwita.    
Askofu Mwita alitumia nafasi hiyo kuihasa jamii kuachana na masula ya Ukatili hasa kwa Wanawake kwani wanapofanyiwa vitendo vya ukatili shughuli mbalimbali za kiuchumi zinakuwa hazifanyiki na hivyo jamii kuendelea kuwa masikini.
Alisema upo ukatili ambao hauzungumziwi sana katika jamii katika suala zima la kumnyima elimu Mwanamke na kudai kuwa hakuna ukatili mbaya kama huo kwani unakwamisha maendeleo.
“Mwanamke lazima apewe elimu pamoja na kumpa nafasi ya kumiliki mali ili aweze kufanya mambo ya faida katika jamii n asiwe Mwanamke wa kuomba kila kitu kwa Mwanaume ikiwa hata kama anataka kununua mafuta ya kupikia ama mboga,”alisema
Kwa upande wake Kaimu Kamanda wa Polisi kanda maalum ya Tarime Rorya Sebastian Zacharia alisema kutokana na askari wanaoshughulika na dawati kupata mafunzo ya namna ya kufanya majukumu yao anaamini watafanya kwa uadilifu mkubwa.
Alisema Jeshi la Polisi limeingia moja kwa moja katika mapambano ya ukatili wa Kijinsia na kudai kuwa jamii inapaswa kushirikiana na Jeshi hilo ili kuweza kutokomeza matukio ya ukatili katika jamii.

No comments:

Post a Comment