Msanii Maarufu na aliyekuwa anakuja kwa kasi katika muziki na pia matangazo ya biashara likiwemo la Airtel Money la kampuni ya simu ya Airtel aliyejulikana kwa jina la Sharobaro a.k.a Sharo Milionea amefariki dunia leo.
Kamanda wa Polisi mkoani Tanga, Afande Constatine Masawe, amethibitisha kutokea kwa kifo cha wa Sharobaro, kufuatia ajali ya gari katika kijiji cha Lusanga, Muheza, mkoani Tanga ambako ndio nyumbani kwao.
Taarifa zinasema kuwa Hussein Ramadhani au Sharo Milionea alikuwa akiaendesha gari namba T478 BVR Toyota Harrier akitokea Dar es
salaam kwenda Muheza alipofika eneo la ajali gari lake liliacha njia na
kupinduka mara kadhaa na kusababisha kifo chake, mwili wa marehemu
umehifadhiwa kwenye hospitali Teule ya wilaya ya Muheza.
Katika eneo hilo inasemekana hakuna kona
kali sana wala ubovu wa barabara kwenye sehemu aliyopata ajali Sharo
Milionea,.
Blog ya Mwana wa Afrika imepokea habari hizi kwa mshtuko na masikitiko makubwa kwani nyota ya Sharo Milionea ndiyo ilikuwa inaanza kung'ara katika anga za muziki pamoja na matangazo ya biashara, akiwa kayapumulia pumzi mpya wa ubunifu na weledi katika kupeleka ujumbe kwa watazamaji ambao wakubwa na wadogo walimpenda.
R.I.P Sharo
No comments:
Post a Comment