Wednesday, September 12, 2012

WANANCHI MUSOMA WALISHANGAA JESHI LA POLISI


MUSOMA

WANANCHI Manispaa ya Musoma mkoani Mara wamelishangaa Jeshi la Polisi mkoani humo kuzuia Maandamano ya Amani ya Waandihi wa Habari hapo jana .

Wakiongea kwa Nyakati tofauti mjini Musoma,wananchi hao wamesema kuwa waandishi wa habari walitaka kuandamana ikiwa ni njia ya kupinga mauaji ya mwandishi mwenzao Daud Mwangosi ambayo yamesababishwa na Jeshi hilo.

 Walisema Askari Polisi wanatakiwa kulinda amani na si kuzuia maandamano hayo kwani wangekubali kuandamana kwa waandishi hao nini ambacho kingetokea huku waandishi hao hawazidi hata 50 ina maana hao Askari hawawezi kulinda watu hao.



  “Mimi jana nimeshangaa sana Askari Polisi kukataza Maandamano ya Amani ya waandishi wa Habari,hawa jamaa walikuwa wanapinga kuuawa kwa Mwenzao sasa inakuwaje hawa jamaa wanawazuia” alisema Mzee Jacob Daniel

Alisema kitendo kilichifanywa na jeshi la polisi mkoani hapa si cha kiungwana hata kidogo kwani maandamano hayo hayakuwa na uvunjifu wa amani isipokuwa kulani kitendo cha mauaji ya mwandishi mwenzao kilichotokea mkaoni Iringa.

Mariam  Chacha alisema kitendo cha jeshi hilo kuzuia maandamano hayo ni dhahiri kuwa wanaunga mkono kitendo cha ukatili kilichofanywa na wenzao mkoani Iringa.

Alisema  wananch hatuungi mkono kitendo hicho hata kidogo”kwakweli tunamshangaa mkuu wa polisi mkoani hapa kutumia madaraka yake kuwanyima waandishi haki yao ya msingi ya kufanya maandamano ya amani kupinga mauaji ya mwandishi mswenzao aliyeuwawa kikatili bila hatia’’alisema Chacha.

Juma  Mafuru alisema polisi wameshindwa kuzuia makundi ya uhalifu yanayosumbua wananchi kwa kuwaibia mali zao,kuwakata mapanga .
Mafuru alisema makundi hayo yamekuwepo mjini hapa kwa muda mrefu wananchi wamejawa na hofu na makundi hayo.
Hata hivyo aliyataja makundi hayo yaliyoshindwa kudhibitiwa na jeshi hilo yenye majina ya ajabu kama vile jamaika moka na mbio za vijiti.

Mapema hapo jana majira ya saa moja asubuhi katika ofisi za Chama cha Waandishi wa Habari Mkoani Mara (MRPC) Waandishi kutoka Wilaya za Mkoa huo walianza kuwasilia kwa ajili ya kutekeleza suala la kuandamana kulaani maauji hayo ya kinyama kwa Mwaandishi huyo wa Habario wa Mkoani Iringa.

Waandishi wakiwa katika mnaandalizi ya kuanza maandamano hayo majira ya saa mmbili na nusu alifika katika ofisi hizo OC CID wa Wilaya ya Musoma Mahamudi Banga kwa niaba ya Mkuu wa Polisi ya Wilaya ya Musoma akiwa na barua yenye kumbukumbu MUS/A.3/VOL 11/.378 ikitaka kuzuia maandamano hayo kwa kwa kile kilichoelezwa katika barua hiyo kuvunja kifungu namba 43(1)ya Polisi na wasaidizi Polisi 2002 ya kutoa taarifa kwa masaa 48.

Katika maandamano hayo Waandishi wa Habari Mkoani Mara wakiwa na mabango walipanga kupita katika
 barabara za kusaga-Nyerere kupitia NMB na kurudi katika ofisi za chama hicho zilizoo katika jengo la Bodi ya pamba.

No comments:

Post a Comment