Saturday, July 21, 2012

GREDA LAGONGA MWENDESHA PIKIPIKI MJINI MUSOMA JIONI YA LEO NA KUSABABISHA KIFO

 
Ajali mbaya iliyohusisha Greda na Bodaboda imetokea leo mjini Musoma katika makutano ya Barabara ya Shabani na Bus Stop.
 
 Ajali hiyo imepelekea abiria aliyekuwa amepakiwa katika pikipiki hiyo kujeruhiwa vibaya maeneo ya tumbo baada ya kuburutwa na mashine hiyo ya kutengenezea barabara.
 
Hata hivyo limetokea gari la shirika la umeme Tanesco na kumchukua majeruhi huyo na kumkimbiza katika hospitali ya Mkoa wa Mara. 
 
Mpaka mwandishi wetu anaondoka eneo la tkio kulikuwa na sintofahamu ya ni wapi dereva wa pikipiki na greda hilo walipoelekea kwani mashuhuda wa tukio hilo wanasema dereva wa pikipiki alikimbia punde tu ajali ilipotokea.
 
Taarifa ambazo Mwana wa Afrika amezipata na kuthibitishwa na baadhi ya Marafiki ni kwamba dada huyo amefariki dunia muda mfupi baada ya kufikishwa hospital
 


No comments:

Post a Comment