Thursday, August 4, 2011

WAZIRI WA HABARI DKT EMMANUEL NCHIMBI AZINDUA BODI MPYA YA MCT

WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Emmanuel Nchimbi akizungumza na wajumbe wa Bodi mpya na ya zamani ya Baraza la Habari Tanzania(MCT), wakiwemo na wadau wengine wakati wa uzinduzi wa bodi hiyo uliofanyika jana jioni katika hoteli ya Courtyard jijini Dar es Salaam.
WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel (kulia) Nchimbi akimkabidhi cheti cha utendaji kazi mzuri katika kipindi cha bodi iliyopita Rais wa Baraza la Habari Tanzania (MCT), Jaji Robert Kisanga, wakati wa uzinduzi wa bodi mpya uliofanyika jana jioni katika hoteli ya Courtyard jijini Dar es Salaam.Jaji Kisanga amendelea pia kuwa Rais wa MCT.
WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Emmanuel Nchimbi wanne kutoka (kulia) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi mpya na ya zamani ya Baraza la Habari Tanzania(MCT), wakati wa uzinduzi wa bodi mpya uliofanyika jana jioni katika hoteli ya Courtyard jijini Dar es Salaam.
WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Emmanuel Nchimbi (kulia) akimpongeza Mhariri wa gazeti la Nipashe Jumapili, Flora Fwingia kwa uhodari wake wa kuandika makala, ambaye pia alikuwa ni mjumbe wa Bodi ya zamani ya Baraza la Habari Tanzania(MCT), wakati wa uzinduzi wa bodi mpya uliofanyika jana jioni katika hoteli ya Courtyard jijini Dar es Salaam.
WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Dkt. Emmanuel (kulia) Nchimbi akimkabidhi vitendea kazi mjumbe wa Bodi mpya ya Baraza la Habari Tanzania (MCT) Bi. Badra Masoud kushoto na katikati ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania(MCT),Kajubi Mukajanga. Makabidhiano hayo yalifanyika wakati wa uzinduzi wa bodi hiyo uliofanyika jana jioni katika hoteli ya Courtyard jijini Dar es Salaam.
WAZIRI wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dkt. Emmanuel Nchimbi (kulia) akifafanua jambo kwa Alex Mgongolwa ambaye alikuwa mjumbe wa Bodi ya ya zamani ya Baraza la Habari Tanzania(MCT), wakati wa uzinduzi wa bodi mpya uliofanyika jana jioni katika hoteli ya Courtyard jijini Dar es Salaam.
  
Source FullShangwe 

No comments:

Post a Comment