Thursday, August 16, 2012

 SERIKALI :VIWANGO VIPYA VYA SUMATRA NDIVYO VITAKAVYOTUMIKA.

Dinna Maningo,Tarime

SERIKALI imesema kuwa viwango vipya vya nauli vilivyotolewa na Mamlaka ya usafirishaji  majini na Nchi kavu SUMATRA ndivyo vitakavyotumika katika magari yanayofanya  usafirishaji wa Abiria ndani ya Wilaya ya Tarime hadi Musoma nakwamba mgomo wa siku mbili uliofanywa na wamiliki wa magari si halali bali ulikuwa  ni kuwatesa wananchi.

Hayo yamebainika kwenye kikao  cha utatuzi  wa mgomo wa wamiliki wa magari Tarime  wa magari yao kutofanya usafiri Wilayani Tarime hadi Musoma Kilichofanyika ndani ya ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Tarime kilichowakutanisha wawakilishi wasafirishaji,baadhi ya viongozi wa Polisi,Ofisa Mfawidhi wa SUMATRA Mkoa wa Mara Maico Rojasi na Mkuu wa Wilya ya Tarime John Henjewele.

Mkuu wa Wilaya ya Tarime John Henjewele alisema kuwa  kikao kimebaini kuwa wasafirishaji walikuwa na mgomo wa kutotoa huduma  ya usafiri na kwamba wamiliki walifanya mgomo kabla ya kutoa malalamiko yao ofisi ya Mkuu wa wilaya na kwamba  mgomo ni batiri kwakuwa  hakuna taasisi yoyote inayotoa magari ya uisafirishaji  iliyosajiriwa kisheria  Richa ya wao kufanya mgomo hivyo viwango vipya ndivyo vitakavyotumika

“Tumefanya kikao na wawakilishi wa usafirishaji wakiwamo baadhi ya viongozi wa Serikali kikao kimebaini kweli kulikuwa na mgomo wa siku  2 wamiliki wenyewe wamekili makosa yao, pia wakati wa mgomo wao hawakuijulisha Serikali bali wamekuwa wakiwasiliana na Sumatra Pekee na mgomo huo ni wa makundi na wala taasisi zao za magari ya usafirishaji hazina usajiri kwahiyo viwango vipya vya serikali viendelee kutumika watakaokiuka watawajibishwa kisheria”alisema Henjewele.

Ofisa Mfawidhi wa mamlaka ya usafirishaji majini na nchi kavu SUMATRA Mkoa wa Mara Maico Rojasi alisema kuwa kwa yale magari madogo maarufu kama mchomoko yanatakiwa kutotoa huduma ya usafilishaji na kwamba yanatakiwa kufanya kazi kwa kukodiwa kama vile Tax kwakuwa ndiyo vyanzo vikubwa vya nauli kupanda na kwamba uamuzi huo hauwazuii wao kuomba kuongeza kupandishwa kwa viwango iwapo wanasababu za msingi.

Kwa upande wa wawakilishi wasafirishaji  wakiwakilishwa na katibu wao Stephano Keraryo wamekili kuwa na mapungufu likiwamo la kufanya mgomo bila kuifahamisha Serikali hususani Mkuu wa Wilaya ya Tarime John Henjewele na chama chao cha wasafirishaji kutokuwa na usajiri ambapo wamekubali kuendelea na huduma ya usafirishaji kwa viwango vipywa wakati huo wakifanya taratibu zingine za kuomba kupandishwa kwa nauli

No comments:

Post a Comment