Na Pascal Michael,
Musoma
Kundi linalosadika ni al shabaab la nchini Somalia llaingia nchini Tanzania na kuondoka na watanzania
wanane waishio buhemba katika wilaya ya butiama mkoani mara na kufanikiwa kuwashawishi
na kuwapeleka nchini
Ethiopia katika migodi ya uchimbaji wa madini
ya dhahabu na kuambulia
mateso makubwa .
Wasomali hao walikuwa wawili
huku wakiwa na gari lao ambalo
halikuweza kufahamika ni aina gani ndipo
walipotinga katika mgodi wa wachimbaji
wadogo wa madini ya dhahabu kijijini
hapo na kufanikiwa kuongozana nao watu hao wanane wakiwa na matumaini ya kwenda kutajirika wakiwa nchini Ethiopia kumbe walikuwa
wakifurahia mateso..
Inadaiwa kuwa watu hao
walikwenda kijijini hapo wakiwa na mwenyeji wao aliyejulikana kwa jina moja la
Nyambura mkazi wa Tarime ambaye alikuwa nafanya biashara ya kuchoma nyama.
Akizungumza na waandishi wa
habari jana, Chaku Maduhu Mkazi wa Bariadi Mkoa wa Simiyu ambaye ni mchimbaji
wa dhahabu katika mgodi wa Buhema alisema kuwa walikubaliana na watu hao kasha
kuambatana nao kuelekea Tarime tayari kwa kuvuka mpaka kuingia nchini Kenya
walikuwa na gari.
“Baada ya kufika mpakani yule
mwenyeji wao alipatiwa fedha kiasi cha sh. Laki tano kasha kurudi Tarime hapo
tulibadilisha gari na kuingia kwenye gari nyingine na kuvuka mpaka na kuanza
safari ya kwenda Ethiopia,”alisema
Maduhu.
Alisema kuwa walipofika
nchini Kenya kijiji cha
Myare ambayo ilikuwa kama kambi ya kukutana kasha walibadilishiwa usafiri na
kupanda pikipiki kuelekea maporini kwa safari iliyochukua takribani masaa manne
hadi kufika kambi iliyoandaliwa nchini Ethiopia.
“Tulipofika huko tulikutana
na watanzania wengine ambao tayari walikuwa wameshatekwa kisha tuligawanishwa
kwenye makundi na kupewa kibarua cha kuchimba madini,”alisema.
Alisema kuwa katika eneo hilo ambalo walikuwa
wanachimba madini walikuwa wanakutana na mabaki ya risasi na mabomu
alipowadadisi watanzania wenzake walidai kuwa msitu huo ni mwanzo kuna mistu
mingine mbele.
“Niliamua kuwadadisi
watanzania wenzangu walisema kuwa hapa ni mwanzo kuna msitu mwingine mbele
ambako kuna mafunzo ya kijeshi ambapo nilijua kuwa hicho ni kikundi cha Al
shabab cha nchini Somalia,”alisema.
Alisema kuwa watanzania
wenzake walimuambia afanye kila liwezekanalo atoroke ili aweze kufikisha ujumbe
kwa serikali ya Tanzania ili
kuweza kuwasaidia watanzania hao kuwakwamua kwenye kundi hilo kwani wenzake walishindwa kutokana na
afya zao kudhoofu .
“Mimi nilifanikiwa na
wenzangu watatu kutoroka siku ambayo wasomali walikwenda kuabudu misikitini
hiyo ndio ikawa nafasi yetu hadi nchini ambako tulikutana na mtanzania
aliyetusaidia kuwasiliana na ndugu zetu ambao walitutumia nauli ya kurejea Tanzania,”alisema.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa
Mara, Absalom Mwakyoma alipoulizwa juu
ya suala hilo alikiri kijana huyo alifanya mahojiano na mkuu wa upelelezi wa
Mkoa huo Emmanuel Lukula na kusema kuwa wanalifanyia kazi suala hilo ili kupata
ukweli wa jambo hilo.
“Tumelipokea lakini tuanpenda
kuwatahadharisha wananchi kuwa makini na wageni wanaoingia nchini ambao
hawawajui na kuwarubuni,”alisema
No comments:
Post a Comment