Thursday, July 5, 2012


AENDA JERA MIAKA 20  KWA KUPATIKANA NA BUNDUKI SMG.

Dinna Maningo,Tarime

MAHAKAMA ya Wilaya ya Tarime Mkoani Mara imemuhukumu Mariba Chacha Kesabo mkazi wa Kijiji cha  Kangariani Kata ya Itiryo kwenda jera kifungo cha miaka 20 baada ya kupatikana na Bunduki aina ya SMG na Risasi 14.

Akitoa hukumu Hakimu Mkazi  wa mahaka ya  Wilaya ya Tarime Yusto Ruboroga alisema kuwa kutokana na mahakama kusikiliza pande zote mbili Mahakama inamtia hatiani Mariba Gesabo kwa makosa mawili ambapo kosa la kwanza ni  kupatikana na Bunduki aina ya SMG yenye namba 052619 ambapo alihukumiwa kifungo cha miaka 10 jera.

Kosa la pili ni kupatikana na risasi 14 ambapo alihukumiwa pia kifungo cha miaka 10 nakwamba adhabu zote mbili zinaenda kwa pamoja .

Upande wa mashitaka ulipokea mashahidi 3,shahidi wa kwanza aitwaye Askari No.G 7055 D/C James,Mwita Athumani ambaye ni mwenyekiti wa Kitongoji cha Bilandi kijiji cha Kangariani na shahidi wa tatu alikuwa ni Askari No. D8661 D/CPL Halson ambapo upande wamshitakiwa hapakuwa na shahidi 

Awali ilidaiwa na mwendesha mashitaka wa polisi Sagent Abel Kazeni  kuwa mnamo tarehe 3 Desemba 2011 majira ya saa 7 na nusu mchana alipatikana  na hivyo vitu nyumbani kwake akiwa amevificha kwenye shamba lake la migomba lililoko eneo la nyumbani kwake.

Hata hivyo mshitakiwa alijitetea kwamba  bunduki hiyo alipewa na rafiki yake Marwa Maico aishiye Nchini Kenya siku ya tarehe 28/7 2011 kwamba ataifata baadae
Mshitakiwa alipopewa nafasi ya kujitetea ili apunguziwe adhabu baada ya kupatikana  na hatia  hakusema chochote.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,MWISHO,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,


AHUKUMIWA JERA MWAKA MMOJA KWA WIZI WA GUNIA MBILI ZA MCHELE.

Dinna Maningo,Tarime

MAHAKAMA ya Mwanzo Tarime Mjini Mkoani Mara imemuhukumu John Nyamanyi kwenda jera kifungo cha mwaka mmoja baada ya kupatikana na hatia ya wizi wa magunia mawili ya mchele  kila moja lenye ujazo wa zaidi ya kilo 80 ambapo anatakiwa kulipa fidia ya kurejesha magunia hayo au pesa zenye thamani ya kiasi cha mchele pindi atakapomaliza kutumikia kifungo.

Akitoa hukumu Hakimu Mfawidhi wa Mahakama ya Mwanzo Jorome Mjini Tarime Migera alisema kuwa Mahakama inamtia hatiani John Nyamanyi baada ya Mahakama  katika kupitia ushahidi wa pande zote Mahakama imeamini mshitakiwa ana hatia kwa kuiba mchele sokoni kwani, baada ya kukamatwa mshitakiwa alidai ametumwa na Marwa  ambapo aliomba kwenda kumuita aliyemuagiza lakini hakuweza kurudi aliondoka moja kwa moja nakwamba aliyedai kumtuma alikana kuwa hakumwagiza.

Alisema kuwa kwa upande wa mashahidi 3 upande wa mlalamikaji walisema kuwa mnamo tarehe  17 mei 2012 mshitakiwa John Nyamanyi aliiba maginia 3 ya mchele yaliyokuwa yamehifadhiwa chini ya uvungu wa meza ndani ya soko kuu la mjini Tarime ambayo aliyatorosha majira ya saa 12 jioni ambapo hata hivyo gunia moja liliweza kukamatwa na mlinzi wa soko wakati akijaribu kulitorosha na kuhifadhiwa kwa mkuu wa soko.

Upande wa utetezi ulileta shahidi mmoja  ambaye ni mshitakiwa ambaye alieleza kuwa aliagizwa na mwenzie aitwae Marwa ambapo alijitetea nakuomba kupunguziwa adhabu kwa kuwa anafamilia na watoto wanaomtegemea.

Wazee washauri Mahakama ya mwanzo  Finias Asumi na Edward Maswi  waliomba mshitakiwa ahumkumiwe kifungo cha mwaka mmoja pamoja na kulipa fidia ya maguni 2 ya mchele ili iwe fundisho kwa wengine ambapo Hakimu Migera aliunga mkono na hivyo Mahakama kumtia hatiani kwa mujibu wa kifungu 265 na kanuni ya adhabu no.16 na kumuhukumu kifungo cha mwaka mmoja jera pamoja na faini ya kurejesha magunia mawili ya mchele na kwamba haki ya rufaa iko wazi mbele ya mahakama ya Wilaya ya Tarime.
,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,MWISHO,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,

No comments:

Post a Comment