SERIKALI wilayani Bunda mkoani Mara imetoa siku tatu
kwa maafisa watendaji wa vijiji,kata na vituo vyote vya polisi wilayani
humo,kuwakamata watu ambao wameanza kulangua zao la pamba kwa wakulima
kinyume na taratibu.
Agizo hilo limetolewa na mkuu wa wilaya ya Bunda Bw
Joshua Mirumbe,kwa nyakati tofauti wakati akiongea na wananchi wa vijiji vya
tarafa ya Chamriho katika ziara ya kujitambulisha baada ya kuteuliwe kushika
wadhifa huo Rais Jakaya Kikwete.
Awali wananchi wa vijiji hivyo wamemueleza mkuu huyo
wa wilaya kuwa kutokana na kuchelewa kufunguliwa kwa msimu wa pamba na ugumu wa
maisha wananchi wameanza kuuza pamba yao kwa walanguzi ambao wamekuwa
wakilangua kwa shilingi 500 kwa kilo moja.
Wamesema wameamua kufikia uamuzi huo kutokana na bodi
ya pamba kuchelewa kutangaza bei halisi ya zao hilo na tarehe maalum ya kuanza
kwa msimu wa pamba ambayo ni zao tegemezi kwao.
Kufuatia malalamiko hayo mkuu wa wilaya, amesema
kuwa msimu wa pamba tayari umeshatangazwa na bei elekezi ambayo makampuni
yanatakiwa kununu kwa shilingi 650 kwa kilo na kwamba wakulima hawapaswi kuuza
chini ya hapo kwa walanguzi hao.
Amesema kuwa kitendo cha walanguzi kupita vijijini na
kuwahadaa wakulima na kuwapa bei ndogo ni kosa la jinai na hivyo akawaagiza
viongozi hao kuwakamata mara moja na kuwafikisha kwenye vyombo vya dola wale
wote watakaobainika kufanya hivyo kuanzia sasa.
Hata hivyo amewaomba wananchi hao kuhakikisha hawaweki
pamba yao maji na magadi kwani kwa kufanya hivyo watakuwa wanaharibu ubora wa
pamba na kufanya ikose ubora katika soko la dunia.
No comments:
Post a Comment