Monday, July 30, 2012

         MWALIMU WAGOMA MKOANI MARA 
                            Wanafunzi washinda wakicheza katika maeneo ya shule

MUSOMA

HATIMAYE walimu wa shule za msingi katika Manispaa ya Musoma mkoani Mara,wameteleza mgomo ulitangazwa na chama cha walimu Tanzania CWT katika kuishiniza serikali kuboresha maslahi yao na mazingira ya kufanyia kazi.


Zaidi ya shule 30 za  msingi katika 44 na sekondari 9 katika ya 18 katika Manispaa ya Musoma hazina walimu kuanzia leo asbuhi huku ofisi za nyingi za walimu na za walimu wakuu zikiwa zimefungwa kwa makufuli.'



Aidha katika baadhi ya shule hizo licha ya kuwapo na wanafunzi lakini zikiwa na mwalimi mmoja hasa mwalimu mkuu,ambao hawakuwa tayari kuzungumzia hali hiyo.


Baadhi ya walimu wamekizungumza kwa njia ya simu wakiwa  majumbani,wamesema wamelazimika kugoma baada ya kuridhishwa kuwa mgomo huo umefuata taratibu zote za kisheria na kwamba wako tayari kwa lolote hadi serikali itakapokubali kuboresha maslahi yao.


Taarifa kutoka wilaya ya Bunda,Serengeti,Butiama zinasema hali ni hiyo hiyo huku wilayani Tarime licha ya walimu kugoma pia wanafunzi  wa shule maeneo ya mjini wamejipanga katika bara bara kwaajili ya kufanya maandamano kwenda katika ofisi ya mkuu wa wilaya ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono mgomo wa walimu wao.

Kutoka Tarime ,Dinna Maningo

KATIKA hali isiyo ya kawaida Wanafunzi wa Shule mbalimbali za Msingi Wilayani Tarime wameandamana hadi ofidi ya Ofisa elimu Wilaya ya Tarime Mkoani mara wakidai haki zao za kupata elimu baada ya walimu wao kugoma kuingia madarasani na kisha kuwataka wanafunzi kuondoka kwenda majumbani kwao .

Wanafunzi hao walisikika wakiimba na kuongea  mbele ya Ofisa elimu wa Wilaya Emanuel Jonson katika viwanja vya ofisi ya elimu Wilaya, walisema kuwa kitendo cha walimu kugoma kufundisha  kinaathiri wanafunzi kwani kwa mgomo huo wanafunzi walio wengi watamaliza shule bila kujua kusoma wala kuandika hivyo wanaitaka Serikali kuwalipa walimu madai yao ili waendelee na masomo.

“Watoto tunataka haki zetu, Watoto tunataka  kupata elimu,  watoto tunataka kusoma tunaomba walimu walipwe madai yao tuingie madarasani ,watoto tusinyimwe haki yetu ya kupata elimu walimu wanapogoma waathirika ni sisi wanafunzi Serikali tatueni mgomo wa walimu” walisema wanafunzi hao.


Ofisa elimu Johnsoni aliwatuliza watoto hao na kuhaidi kutatua tatizo la walimu wao ambapo aliwataka wanafunzi wote kurejea shuleni hapo kesho kuendelea na masomo yao.

Jonsoni alisema kuwa anasikitika kwa kitendo cha walimu kutoingia madarasani na kwamba kitendo hicho ni kupunguza stahili za watoto ambapo  amewataka walimu wote kesho kuhudhulia madarasani na kwamba ambao hawatohudhuria vipindi watawahibishwa .

“Kwa maelezo ya Serikali mgomo ni batiri nimefanya kikao na waratibu elimu wote kuwaelekeza kwenda katani kwao kuwahimiza walimu kurejea shuleni na kwa mujibu wa maelekezo Serikali tumetoa taratibu za kujaza fomu kwa walimu wote za kuthibitisha anaeunga mgomo au asiyeunga mgomo kwa wale ambao watagoma watachukuliwa hatua.”alisema Jonson


“aliongeza” Nasikitika  walimu wamewafanyisha watoto maandamano ,kugoma kunaathiri watoto walimu wasiwanyime watoto haki zao za kupata elimu waendelee kufundisha wakati huo taratibu za Serikali zikifanyika, uzuri kwa Wilaya yangu walimu hawadai madeni wanachodai ni posho,nyongeza ya mshahara, na swala hilo ni la kitaifa Lingekuwa ni tatizo la kiwilaya ningetoa kauli siwezi kutoa kauli tatizo ni la kitaifa”alisema Jonson.

Kuandamana kwa wanafunzi hao ni baada ya walimu kutoka katika shule  mbalimbali za msingi Wilayani Tarime kugoma baada ya Serikali kushindwa kutekeleza mahitaji yao ya posho za kufundishia,Nyongeza ya mshahara na posho za mazingira hatarishi ya kazi.

Mwenyekiti wa chama Cha Walimu Wilayani Tarime Matinde Magabe alisema kuwa mgomo huo ni endelevu hadi pale Mwenyekiti wa CWT Taifa atakapotoa tamko na kwamba hata kesho hawatoingia darasani.

“Mgomo ni halali tunataka Serikali itulipe nyongeza ya mshahara kwa asilimia 100%,posho ya kufundishia asilimia 55 kwa walimu wa sayansi na hesabu asilimia 50 ya mshahara kwa walimu wa masomo ya sanaa,posho ya mazingira magumu ya kazi asilimia 30% na mgomo huu ni endelevu”alisema Magabe .

Magabe alisema kuwa Wilaya ya Tarime inajumla ya walimu wapatao 2870 kati yao ni wa shule za msingi,Sekondari na walimu wa chuo cha walimu Tarime.

No comments:

Post a Comment